Aliniambia Ami Hakimu anaekaa kwa da Fatma ndie aliemfanya.
NA FATMA HAMAD-PEMBA
SHAHIDI NAMBA TANO ZUWENA HASSAN
Mohamed ambae ni jirani alieleza Mahkama ya Mkoa Chakechake kwamba,
muathirika alimuambia kuwa aliemfanyia
kitendo hicho ambacho kilimpelekea kulazwa Hospitali, ni ami Hakimu ambae anakaa kwa da fatma.
Shahidi huyo alidai kuwa Julai 15 mwaka jana aliondoka nyumani kwake
yeye na mtoto wake na kwenda Hospitali
ya Abdala Mzee Mkoani kwa ajili ya
matibabu yake ya Figo.
Alidai kuwa baada ya kufika Mkoani mtoto wake alimuaga na
kumwambia anakwenda msalani (chooni ) kujisaidia, nayeye akabakia na kusubiri andike cheti kwa ajili
ya kwenda kwa Daktari.
Aliporudi
msalani yulele mtoto wake alimuambia kuwa alimkuta babayake akiwa amekuja na mtoto wa shangazi yake
Hospitali.
‘’Aliponiambia babayake yuko na mtoto wa shangazi yake
anamatatizo, nilipandisha hadi ngazi ya
juu chumba wanacholazwa watoto nilimkuta
huyo muathirika amelela kitandani,’’anaeleza.
Alieleza
kuwa baada ya hapo aliondoka na kuwafuata wazazi wa mtoto kituo cha Polisi Mkoani kwa ajili ya kwenda
kusikiliza maelezo watakayopewa kituoni hapo.
Aliendelea
kusemakuwa aliporudi kutuo cha Polisi alikwenda
moja kwa moja Hospitali alikolazwa mtoto, na kumuuliza amefanyiwa na
nani kitendo, nakumjibu alifanyiwa na ami Hakimu anaekaa kwa da Fatma.
‘’Nilimuuliza
nani aliekufanya kitendo hicho alinijibu kuwa ni ami Hakim anaekaa kwa da
Fatma,’’aliniambia muathirika mwenyewe alida.
Baada ya
kumaliza kutoa ushahidi wake shahidi
huyo Mwendesha Mashtaka wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka DPP Asya Ibrahim aliiambia Mahkama hiyo ya
Mkoa kwamba walikua wanashahidi huyo
mmoja, hivyo kesi ighairishwe na ipangiwe sikunyengine kwa ajili ya
kusikilizwa.
‘’Mheshimiwa
Hakimu kwa leo tulikua tunashahidi huyo mmoja tu, hivyo tunaomba tuipangie
sikunyengine,’alidai.
Nae Hakimu
wa Mahkama hiyo ya Mkao iliyopo Chake chake Pemba Taki A. Habib ameighairisha kesi hiyo hadi
Februari 18 huku akimtaka mwendesha
mashtaka kuleta mashahidi wengine.
‘’Naighairisha hadi Februari 18 naomba mulete mashahidi
wengine, na mtuhumiwa utaendelea kukaa rumande hadi tarehe hiyo,’’lieleza.
Hakimu Said Hakim (36) mkaazi wa Jondeni Pemba,
Julai 14 mwakajana sa 4: 00 za usiku huko Jondeni wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini
Pemba, kwa kutumia nguvu na bila ya ridhaa yake alimbaka mtoto wa miaka Saba
(7).
Ambapo
kufanya jambo hilo ni kosa kinyume na kifungu cha 108 (1) (2) (e) na 109 (2) vya Sheria nambari 6 ya mwaka 2018
Sheria ya Zanzibar.

Comments
Post a Comment