Zanzibar Hiro yawakaribisha kisiwa cha Pemba, Kilimanjaro Star


NA SALIM HAMAD- PEMBA

Kocha wa  Timu ya Taifa ya Zanzibar,(Zanzibar Hiro)  Ali Bakari Mgazija mara baada ya kuichapa   bao 1- 0  timu ya Kilimanjaro Star,  katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Michezo Gombani, alisema ushindi huo unatokana na maandalizi mazuri walioyoyafanya.

Alisema haukuwa rahisi kuwafunga wapinzani wao kutokana na ushindani uliokuwepo  lakini anashukuru  kwa Vijana wake kufuata maelekezo,  jambo  ambalo  liliweza  kuchangia  kupata ushindi  huo.

Alisema bado ni mwanzo wataendelea kujituma zaidi kuona kila mchezo wanashida,  ili kuhakikisha ubingwa wa Kombe la Mapinduzi katika msimu huu wa mwaka 2025 wanalibeba.

Alisema anafahamu anakabiliwa na kibarua kizito katika mchezo dhidi ya Burkina Faso utaopigwa Jaruary 6 anaamini,  kwa kasi walioyanayo Vijana wake wataweza kuondoka na alama tatu.

‘’Tunashukuru kwa kumaliza salama niwapongeze wachezaji wangu wamecheza Vizuri kwa kufuata maelekezo tuliyowapa, namini kwa mwendo huu utashinda na michezo mengine licha ya ushindani uliopo’’alisema.

Kwa upande wake Kocha  Mkuu wa timu ya Kilimanjaro Star,Ahmed Ali alisema kufungwa kwenye mchezo huo ni kama bahati walioipata wapinzani wao,  pamoja na juhudi walizozifanya  katika kupambana  kusaka  ushindi  lakini haikuwa bahati yao.

Alisema tayari mapugufu yaliyojitokeza atakwenda kuyafanyia kazi na kujipanga na mchezo mwengine, illi  aweze kupata matokeo mazuri,  na kuwataka Mashabiki na Wapenzi wa timu hiyo kutovunjika moyo watashinda mchezo ujao.

Alisema watawasoma wanavocheza wapinzani wao watakaokutananao  kwenye mchezo ujao dhidi ya Kenya, utakaopigwa January 7 kwani  itakuwa  tayari wameshasoma mbinu zao .

‘’Tukubali tumefungwa mchezo haukuwa mgumu kiasi hicho wala haukuwa rahisi ni matokeo ya kimchezo,  lakini tutayafanyia kazi mapungufu  yaliyojitokeza na tutawasoma wapinzani wetu Kenya  tutakao kutananao katika mchezo ujao hata tukicheza nao itakuwa tumesha jipanga’’alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Mgeni Khatib Yahya alisema kufanyika kwa Michuano hiyo Kisiwani Pemba,kunatoa fursa  kwa Vijana katika kuibua Vipaji Mbali Visiwani Zanzibar.

Alisema hata hivyo Vijana watahamasika kujiingiza katika michezo baada ya kuona baadhi ya Vijana wanavyonufaika na Fursa hiyo kama Feisal Salum kwa kuonesha umahiri wake.

‘’Tunampongeza Rais wa Zanzibar,Dk Husein Mwinyi kwa kuleta Mashindano hayo Kisiwani  Pemba, Kwani yanalenga katika kuibua Vipaji Visiwani humu,  na Vijana kuhamasika kujikita katika Sekta ya  Michezo’’alisema Mgeni.


Katika Mchezo huo Bao Pekee liliwekwa kimiani na Mshambuliaji Feisal Salum Abdalla katika dakika 51.



 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI