Ukata wa fedha unavyochangia wanawake kuyaogopa majimbo.
Na Fatma Hamad – Pemba
Nimewahi kugombea
mara moja tu, ila kila
nikifiria kurudi tena jimboni
narudinyuma, kwani sina uwezo kifedha
Simulizi ya Fatma Shaaban Mohamed (51) mkaazi wa Kiuyu
minungwini Wilaya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba,
inatuonesha ukata wa fedha
unavyomkatisha tamaa kuingia tena jimboni katika Uchaguzi wa 2025
Anasema
amegombea Udiwani mwaka 2010 Jimbo la
Wingwi Shehia ya Njuguni Wilaya ya
Micheweni Kaskazini Pemba,
kupitia Chama cha Mapinduzi CCM.
Mama huyo
ambae amezaliwa katika kijiji cha
Machengwe Ziwani, wilaya ya
Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.
Anasema amesomea
taaluma ya uwalimu
ngazi ya Cheti, katika
Chuo cha Ualimu
cha Wiyat kilichopo
Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba,
na ana familia ya watoto saba.
Anasema
ameanza harakati za siasa mwaka
2012 ameshawahi kugombea nafasi
mbalimbali kuanzia ngazi ya matawi, na hata za kwenye Jumuia ya wanawake.
‘’Nimeshawahi
kugombea nafasi nyingi kuanzia kwenye matawi, na hata nafasi ya ukatibu katika
Jumuia ya akinamama ya Chama
changu, ila sikuwahi
kufanikiwa’’, anasema
Hakukata tamaa aliendelea kupambana na kukitumikia
chama, kwa vile alikua ana imani siku
moja ataweza kufanikiwa.
Suala la kufikiria kugombea alipata ushawishi kutoka kwa
walimu wenzake wa Skuli na akashawishika, kwani alikua na ndoto za kua kiongozi
tokea zamani.
Mnamo mwaka
2007 alianza kikamilifu kushuka tawini
na kuanza kufanya shughuli ndogo ndogo za chama.
Fatma anasema mwaka
2010 alijiingiza jimboni na kugombea nafasi ya Udiwani, na kupambana na wanaume
bila ya kua na khofu yoyote.
Katika kundi la watu waliojitokeza kuchukua fomu katika
Chama chao kwa nafasi hiyo ya Udiwani, yeye ndie alieibuka mshindi, na kuingia
kwenye kinyan’ganyiro na kupambana na wapinzani wenzake wa vyama vyengine.
licha ya kuwa
jamii ilimkubali vya kutosha, ila mwisho wa siku alianguka hakuweza kulikamata
jimbo.
‘’Asikudanganye mtu kama huna pesa kwenye Uchaguzi
huwezi ukashinda, na mimi nasubutu kusema, kilichoniangusha ni pesa
tu sio kituchengine,’’anasimulia.
Kwakweli suala la pesa ni tatizokubwa na linawafanya wanawake
wengi warudinyuma kuingia
majimboni na shindwa kugombea.
‘’Sasahivi
wanawake tuliowengi tumekua na
hamu ya kugombea, ingawa umasikini
unatufelisha, kama huna pesa
hakuna yoyote unaempiga kampeni akakuangalia,’’anaeleza.
Amegundua suala la pesa ni silaha kubwa kwenye Chaguzi,
na ndio inayowafanya wenyepesa zao sikuzote kubakia wao kwa wao majimboni, na
masikini kuishia kuwa wapiga debe tu.
Anatamani kurudi tena
jimboni, ila amekata tamaa, kwani ni masikini, hana pesa zitakazomsaidia kufanya shughuli za
kampeni katika kipindichote cha Uchaguzi
FAMILIA YAKE
Kombo Khatib Bakar
(60) mkaazi wa Kiuyu minungwini ni mume wa mwanamama huyo shujaa anasema
baada ya mke wake kumpa wazo la kutaka
kugombea hakumkatalia, alikua
anamuamini ataweza, kwani alikua ni mpambanaji na mpenda maendele.
Alijitoa kihali na mali kumsaidia mke wake huyo kwa kila
alichojaliwa nacho, kuhakikisha anapata
nafasi, ili aweze kuja kuwa msaada kwa
wanawake wenzake na hata kwa Taifa .
‘’Simkumzui wala
sikua na hisia mbaya nae, bali
nilimuunga mkono kwa kipindichote, kwani nilikua namini anaweza
kupambana,’’anafahamisha.
Hivyo amewashauri wanaume wenzake kuwa na uthubutu kama yeye, wawaruhusu wenza wao kuingia kwenye fursa mbalimbali za maendeleo ili walete
mabadiliko kwenye jamii,’’anafahamisha.
Amefahamisha kua walikua wanaimani endapo akapata jimbo ataleta maendeleo kwa wananchi wake,
kupitia Nyanja mbalimbali ikiwemo Afya.
‘’Kiongozi
mwanamke Tunakua na imani nae zaidi, kwani yeye pia ni mama, na siku zote
anaejua utungu wa mwana ni mama mzazi,’’anaeleza.
JIRANI YAKE
Saumu Omar Hamad (40) mkaazi wa Kiuyu minungwini anasema jirani yao huwa anaweza kua kiongozi
nzuri, kwani ni mtu anaekua karibu na wenzake, amekua akiwashauri mambo mengi
ya kimaendeleo.
‘’Kwa Kweli jirani yetu huyo tunamkubali kua kiongozi,
ametuhamasisha tumejiunga katika vikundi vya hisa, ambapo tukiwa na shida zutu
tunakwenda tukikopa,’’amemalizia Saumu.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Wiala ya Micheweni Khamis Juma Omar anasema
wanachokifanya kwasasa ni
kuwasimamia wanawake wa Chama
chao kupata mikopo
serikalini, ambayo itawasaidia
kuendesha shughuli zao za
Uchaguzi.
‘’Tumekua tukiwasimamia na kuhakikisha wanapata mikopo
ya mfuko wa uwezeshwaji wanawake
kiuchumi ili kumudu kuendesha shughuli zao, kwa kipinduchote cha
kampeni,’’anafafanua.
WANAHARAKATI
Hidaya Mjaka Ali mwanaharakati wa masuala ya
watuwenyeulemavu kisiwani Pemba anasema ipo haja kwa Serikali na vyama vya
siasa, kuweka ruzuku maalumu kwa ajili ya kuwawezesha wanawake wanaotaka
kugombea, ili kuona wamejitokeza kwa wingi majimboni katika uchaguzi wa 2025.
Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar kimesema kimekua kikifanya jitihada
mbalimbali, kuona kumekua na mazingira rafiki kwa wagombea wanawake katika uchaguzi
mkuu wa Octobar 2025.
‘’ Tunatamani kuona kumekua na uwezeshwaji wa kifadha kwa
wagombea hususan wanawake, ili wawe na hamu ya kuingia majimboni na kugombea,’’
Amina Ahmed Kaimu Mratibu Ofisi ya TAMWA
Pemba anashauri.
TAKWIMU
Kwa mujibu
wa ripoti ya Tume ya Taifa
ya Uchaguzi
na Kamati ya Kufuatilia Uchaguzi
Tanzania kuanzia 2015
hadi 2020 Idadi
ya Madiwani wanawake wa
kuchaguiwa kutoka kwenye kata
ni 204 ambao
ni sawa na asilimia
5 ya Madiwani wote.
Kwa Zanzibar
idadi ya waliojitokeza
kugombea Udiwani katika
Uchaguzi wa 2020
wanaume walikua 276
wanawake 74 Walioshinda wanaume ni 85 wanawake 25
Kwa mujibu wa Sensa ya
watu na makazi
ya mwaka 2022
Zanzibar inawanawake wengi ambao
ni 974,281 sawa
na asilimia 51.6
kuliko wanaume, ikiwa wao ni 915,492
sawa na 48.4
Ambapo
licha ya uwingi huo bado idadi kwenye ngazi za maamuzi ni kidogo, Kati ya hao,
ni asilimia 21.14 tu kwa wanawake 71 waliojitokeza kugombea udiwani.
ILAANI YA UCHAGUZI YA WANAWAKE.
Ilani ya Uchaguzi
ya wanawake, Uchaguzi wa Serikali za mitaa ya mwaka 2019 na
Uchaguzi mkuu wa
2020, Madai ya mtandao wa wanawake wameitaka serikali kusimamia matumizi ya rasilimali fedha, hususani ruzuku zitokanazo na kodi
ya Watanzania, ili kuhakikisha zinatumika kwa kuziba mapengo
ya jinsia wakati wa uchaguzi.
ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI.
Moja ya mkakati
wa Ilani ya
Chama cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2024
imesema, ni kuwawezesha wanawake kushiriki katika ngazi mbalimbali za mamuzi.
Hata katiba ya Zanzibar
ya 1984 katika kifungu cha 21 (1) kinaeleza
kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika
kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu mwanamke na Taifa lake.
Mkataba wa kikanda wa Nchi za kusini mwa Afrika, uliotiwa saini mwaka 2008 kupitia kifungu
nambari 13 cha mkataba huo,
kinaelezea kuwekwa mikakati
madhubuti ya kuwawezesha wanawake kiuchumi na kuwashajiisha katika
Nyanja mabali mbali za siasa.



Comments
Post a Comment