TAMWA yatoa agizo kwa wandishi wa habari wa pemba


                        Na Fatma Hamad –Pemba

Wandishi wa habari wametakiwa kujikita zaidi vijijini kuibua kero zinazowakwaza wananchi juu  ya masuala ya Afya ya uzazi, ili kuona zinajulikana na kupatiwa ufumbuzi.

Wito huo umetolewa na Afisa ufuatiliaji na Tathmini kutoka Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar Mohamed Khatib Mohamed wakati akizungumza na wandishi wa habari na wafanyakazi wa wizara ya afya huko ukumbi wa Tamwa Chakechake Pemba.

Amesema bado wananchi hususani wanaoishi vijijini wamekua wakikumbana na vikwazo kadhaa kama vile  kukosekana kwa vituo rafiki kwa mama wajawzito pamoja na upatikananji wa huduma bora za afya.

Amesema wandishi wa habari ndio mkombozi wa wasio na sauti, hivyo endapo watafanya  kazi zao ipasavyo na wakaweza kuziibua kero hizo ambazo ni kilio kwa wanajamii, kutasaidia  kupatikana  kwa huduma rafiki na kuepukana na athari zitokanazo na masuala ya afya ya uzazi.

‘’Wandishi wa habari nendeni vijijini mkandike shida za wananchi ili zipate kutatuliwa,’’amesema.


Kwa upande wake Mratibu wa Kitengoshirikishi Kifua kikuu, Ukimwi, Homa ya ini na Ukoma upande wa Pemba Khamis Hamad Ali amewasisitiza wandishi wa habari kuendelea kuielimisha jamii kujitokeza kwa wingi vituo vya afya kupima afya zao, ili waweze kupatiwa tiba mbadala sambamba na kuwaepusha kuwambukiza virusi  wengine.

Amesema takwimu zinaonesha kua wengi wanaopata mambukizi ya Virusi vya Ukimwi  ni vijana kuanzia miaka 15 hadi 35.

‘’Wengi wanaoambukizwa Virusi vya ukimwi ni vijana, hivyo ni vyema vijana mkajitokeza kwa wingi Hospitali kupima afya zenu,’’anashauri.


Nae Khairat Haji kutoka Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa Zanziar amewataka wafanyakazi wa wizara ya afya Pemba kushirikiana na wandishi wa habari katika  kuielimisha jamii juu ya masuala ya afya ya uzazi, ili kuona kunaibuliwa changamoto zinazoikwaza jamii juu ya masuala hayo.

 



 

Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO