Mitazamo finyu ya jamii inavyowakosesha fursa za uongozi, wanawake
Na Fatma Hamad-Pemba
Kwa mujibu wa Sensa ya
watu na makazi
ya mwaka 2022
Zanzibar inawanawake wengi ambao
ni 974,281 sawa
na asilimia 51.6
kuliko wanaume, ikiwa wao
ni 915,492 sawa na
48.4 ambapo licha
ya uwingi huo bado
idadi kwenye ngazi
za maamuzi ni
kidogo.
licha ya uwingi huo bado idadi ya wanawake
wanaojitokeza na kugombea Kati ya hao,
ni asilimia 21.14 tu kwa wanawake 71 waliojitokeza kugombea udiwani.
Kwa nafasi ya uwakilishi
wanawake waliogombea ni 251, wakiwemo wanaume 190 na wanawake 61, ambapo
walishinda wanaume 42 na wanawake nane (8) sawa na asilimia 16,
wabunge walioshinda wanawake ni wanne sawa na asilimia 8,
Hata katiba
ya Zanzibar ya 1984 katika kifungu cha 21 (1) kinaeleza kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki
kikamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu mwanamke na Taifa lake.
Hata Sera
na Sheria mbalimbali
za Zanzibar zimeelekeza
kutambua haki ya
mwanamke kushiriki katika
demokrasia na uongozi.
Ijapokua wanawake wamepewa fursa ya kugombea na kushika nafasi mbalimbali za mamuzi, lakini bado Jamii inaonekana haikotayari kuwachagua viongozi wanawake, na hii ni kutokana na mitazamo finyu inayojengeka kwa wananchi.
Hivyo basi
Makala hii imezungumza
na wananchi pamoja na wadau mbalimbali kisiwani
Pemba na kutaka kufahamu, ni kwanini Jamii
haikotayari kuwachagua viongozi wanawake.
SABABU ZINAZOPELEKEA
JAMII KUTOKUWACHAGUA VIONGOZI WANAWAKE
JAMII
Fatma Mohamed
Shaaban mkazi wa Penjewani wilaya ya Wete Pemba, anasema jamii iko tayari kuwachagua viongozi
wanawake, ila kinachowatia hofu kuwachagua, ni kwamba wengi wanaogombea hawana
sifa.
Anasema
wanawake wengi hawana utayari, na wengi wao hawashiriki kwenye vikao vya vyama.
‘’Wale wanawake wenye sifa hasa na wenye uthubutu wa
kusimama mbele za watu na kuweza kutetea mambo ya kimaendeleo, hawajitokezi
kusimama majimboni na kugombea’’, anaeleza.
Juma Kombo
Hija mkaazi wa Micheweni anasema jamii haikotayari kuwachagua viongozi wanawake,
kwa sababu waliowengi hawataki kuongozwa na wanawake.
‘’Hadi leo
wapo baadhi ya watu wanamawazo finyu,
hawapendi mwanamke ashike nafasi
ya juu, wanataka sikuzote wawe ni watu wa kukaa mkiani,’’anaelza.
Fatma Rashid mkaazi wa Sizini wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba anasema Jamii hawako tayari kuwachagua viongozi wanawake, kwa sababu bado hao wanawake wenyewe wanasuasua, hawajakua kitu kimoja juu ya masuala ya uongozi.
‘’Tulitarajia
anaposimama mwanamke mwenzetu jimboni ashinde,
kwa sisi wanawake tuko wengi ni , lakini
chakushangaza hata sisi wenzake tunamsaliti,
tunawafanya wanaume kilan siku kua mbele
wao,’’anasema.
VIONGOZI
WA VYAMA VYA SIASA
Maryam Saleh
Juma ni Mwenyekiti wa Mkoa wa Chama cha
Ukombozi wa Umma (CHAUMA) anasema jamii wanaogopa kuwachagua wanawake,
wanadai kua hata wakiwachagua hawapati nafasi.
‘’Hata
mwanamke akashinda anapigwa vita alimradi asipite, wanaume bado hawajawakubali
wanawake kushika uongozi,’’anaeleza.
Abass Mohamed
Khatib Mratib wa Chama cha Demokrasia Makini (DP) anasema jamii haikotayari kuwachagua viongozi wanawake kwa sababu wengi wanaogombea hawana uwezo wa
kusimamambele za watu na
kuzungumza.
Anasema wengi
wa wanawake hawashuki chini kwenye matawi na kufanya shughuli za chama na
kuweza kujijengea uzoefu.
‘’Wengi
wa wanawake wanajificha wanasubiri
kipindi cha uchaguzi ndo wanakuja
majimboni kwa kujaza
fomu tu za kugombea, hawana ule uzoefu wa kuzungumza
na watu,’’anafafanua.
Anasema jamii
inahitaji mtu ambae ataweza kusimama na kuwatetea shida zao, na sio
kuchagua kiongozi kwa kua ni mwanamke mwisho wa siku akaishia mpiga kofi kwenye
meza.
WANASHERIA
Khalfan Amour
Mohamed mwanasheria wa kujitegemea kutoka wilaya ya Chakechake
Mkoa wa Kusini Pemba, anasema wanchi hawakotayari kuwachagua viongozi
wanawake, kwani wengi wa wanawake wanaogombea hawana sifa za kugombea, hawashiriki
ipasavyo shughuli za chama.
Anasema
wanawake walio na sifa za kugombea hawajitokezi matawini na kushiriki harakati
za kwenye vyama wakaweza kuonekana.
‘’Kiukweli hasa wale
wanawake wasomi wenye
uthubutu hawajitokezi kwenye shughuli za vyama, wanajificha, wanawahamasisha wengine
kugombea ambao hawanasifa, jee wananchi watawachagua, anasema khalfan.
Anasema ipo
haja kuwekwa mifumo mbadala kwenye siasa ili kuona wanawake walio na elimu
wanajitokeza kwenyeshughuli za vyama bila ya khofu, jambo litalopelekea kupata
nafasinyingi za uongozi kwa wingi.
Saleh Hamad Juma ni
kaimu Mkurugenzi wa Jumuia ya wasaidizi wa Sheria
wilaya ya Micheweni Mkoa wa
Kaskazini Pemba, anasema
yeye anaona kiongozi
mwanamke ni bora kwani
sikuzote anaejua utungu wa mwana ni mama.
‘’Tukiangalia hata Raisi wetu
wa mungano ni mwanamke, na tunamuona anvyofanya vizuri licha ya uwanawake wake maendeleo yanapatikana,’’amefafanaua.
WANAHARAKATI
Semeni Ali
Khamis mwanaharakati wa masuala ya wanawake na watoto Wilaya ya Micheweni anasema, ili kufikiwa lengo la
hamsini kwa hamsini
ya uongozi. ipo haja kwa wanawake
kukaakitu kimoja na kuungana mkono,
kuhakikisha wanaingia kwa wingi majimboni katika
Uchaguzi mkuu wa
2025.
Amina Ahmed
Mohamed ni kaimu Mratibu wa Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania
Zanzibar (TAMWA ) Ofisi ya Pemba, anasema wamekua wakitoa elimu siku hadi siku kwa wanawake
juu ya masuala ya uongozi, ili kuona
wanakua kitu kimoja, na kuona wanajichukulia nafasi mbalimbali za
maamuzi.
WACHAMBUZI WA MASUALA YA HABARI
Bakar Mussa
Juma ni mwenyekiti wa Jumuia ya wandishi wa habari kisiwani Pemba anasema
kiongozi mwanamke ni bora kwani, maranyingi yeye ndo anakua karibu zaidi na
Jamii.
‘’Mara nyingi
mwanamke yeye ndo anakua karibu na wananchi, inakua ni rahisi kuzifahamu shida
zinazowamkubwa,’’anafahamisha.

Comments
Post a Comment