Hemedi alitwisha mzigo shirika la Nyumba la Zanzibar
Na Fatma Hamad- Pemba
Makamo wa pili wa Rais wa
Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla
ameliagiza Shirika la Nyumba kuendelea kujenga majengo ya kisasa
katika mji wa Chakechake, ili uweze kuendena na mazingira ya sasa.
Makamo huyo
ameyasema hayo wakati akifungua Nyumba za biashara na maakazi huko Mkungumalofa
Chakechake Mkoa wa Kusini
Pemba.
Amesema Serikali ya awamu
ya nane, imedhamiria kujenga majengo ya
kisasa katika miji
yote ya Zanzibar, ili kuona wananchi
wake wanaishi katika majumba zenye hadhi na zenye kuvutia.
‘’Chakechake ndio mji mkuu wa Pemba, nikuombe waziri wa
Ardhi kuhakikisha Chakechake imebadilika, nakua mji wa kisasa,’’ameagiza.
Amesema
majengo hayo ya kisasa yatawanufaisha wananchi kupata makaazi bora, pamoja na wafanyabiashara wote, hivyo ni budi jamii
kutoa mashirikiano na Serikali ili kuona majengo hayo yamesimama.
Aidha amewataka wananchi kuendelea kudumisha amani na utulivu, ili Nchi izidi kupiga hatua kimaendele.
Mapema waziri wa Ardhi nyumba na makaazi Zanzibar Rahma Kassim Ali amesema, wataendelea kujenga majengo ya kisasa, kili kuona miji yote ya Zanzibar inakua na hadhi.
Akitoa tarifa ya kitaalamu Katibu mkuu
wizara ya Ardhi na maakazi Zanzibar Khadija Khamis Rjab
amesema, Jumla
ya shilingi Bilioni moja ishirini
na sita zimetumika kwa ajili ya
ujenzi huo, ikiwa ni pamoja na kulipwa mjenzi
na mshauri elekezi.
Amesema
nyumba hiyo yenye Gorofa nne inanyumba nane za maakazi zenye vyumba
vitatu, Maduka 20 ilijengwa na Mkandarasi wa kampuni ya Zanzibar
Hause Coporation kwa kupitia mshauri
elekezi wakala wa
majengo Zanzibar ZBS.
Kwa upande
wake Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Rashid Hadid Rashid amesema Mkoa
wake utaendelea kuunga
mkono jitihada za Rais wa Zanzibar,
ili kuhakikisha amani na
maendeleo yanaendelea kupatikana Mkoani humo.
Comments
Post a Comment