Wakulima wa kilimo msitu waomba kupatiwa Pembejeo.
Na Fatma Hamad –Pemba WAKULIMA WANAOLIMA KILIMO MSITU katika Shehia za Mjini kiuyu, Kambini kichokochwe, Mchanga mdogo na Chwale wilaya ya Wete Pemba, waomba kupatiwa vitendea kazi ikiwemo Miche ili waweze kuendeleza kilimo chao hicho. Wakizungmza na mwandishi wa habari hizi huko vijijini kwao mwananchi Maryam Khamis Bakar na Anu Omar Juma , walisema tayari wamesha tayarisha mashamba yao, ila wameshindwa kupanda kutokana na kukosa miche kwa ajili ya kuotesha. ‘’Tayari tumesha tayarisha mashamba yetu vya kutosha, ila tumeshindwa na Miche,’’walisema. Hivyo waliwataka wizara ya Kilimo maliasili, Mifugo na Uvuvi pamoja Jumuia ya upandaji wa Misitu Pemba CFP kuhakikisha wanawapatia miche ya aina mbalimbali ili waweze kuotesha katika mashamba yao hayo. Kwa upande wao wakulima Aisha Khamis na Suleiman Abdala Hamad wanasema kilimo msitu kitawafanya wanawake kupiga hatua...