Wanawake wawagaragaza wanaume, katika kamati za uhifadhi mazingira za shehia

 


                        Na Fatma Hamad- Pemba

Rais Samia Suluh Hassan wa Tanzania, mara baada ya kula kiapo Machi 19, 2021, alitaja moja ya vipaumbele vyake, ni kuyashirikisha makundi mbali mbali wakiwemo wanawake.

Na ndio maana wapo mawaziri kadhaa wanawake wanaoongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwemo waziri wa Afya Jenister Mhagama, na mwenzake  Ashatu Kijaji anashikilia wizara ya Mifugo na uvuvi.

Lakini hata wizara ya Fedha na mipango, inashikiliwa na mwanadada  Natu Elmaamry Mwamba kwa nafasi ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo.

Eneo jingine ni uwepo wa sera ya taifa ya Jinsia na maendeleo ya mwaka 2023/2033 ambayo nayo imehimiza, uzingatiaji wa haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake na wanaume.

Kwa Zanzibar katiba ya mwaka 1984, kifungu cha 10 (e) kimeleza kila raia atakuwa na haki sawa, majukumu na fursa sawa kwa mujibu wa sheria.

 Ndani ya bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Wwatoto Zanzibar ya mwaka 2024/2025 ikaubua kuwa, tafiti zinaonesha kuwa nchi zinazozingatia usawa wa kijinsia zimeweza kuimarika kiuchumi kwa kasi kuliko,  ambazo hazizingatii usawa huo.

Kimataifa ripoti ya UN Women na ECOSOC ya Septemba 2023, inatoa wito wa ufadhili kwenye programu za kuhamasisha usawa wa jinsia.

Kwa kuzingatia hilo, wenzetu wa Jumuia ya uhifadhi wa misitu Pemba ‘CFP’ wakishirikiana na wenzao wa kimataifa ‘CFI’ kwa ushirikiano na Chama cha wandishi wa habari wanawake (TAMWA) Zanzibar, katika  mradi wa uhifadhi mazingira, wakalenga  zaidi wanawake, ili kutekeleza azma ya usawa.

UZINGATIAJI USAWA WA JINSI KAMATI ZA HIFADHI YA MAZNGIRA

Kamati za shehia nne za wilaya ya Wete  Pemba, ambapo mradi wa mabadiliko tabianchi, umebisha hodi, utafiti unaonesha utekelezaji wa sera ya jinsia kwa vitendo.

Maana ndani ya kamati hizo, ambazo zinatekeleza  mradi  huo, zimefanikiwa kutekeleza  sera kwa vitendao, kwani  kati ya wajumbe wote 110 wanaounda kamati hizo, wanawake ni 68 sawa na asilimia 0.68 ya wajumbe wote.

Kwenye shehi hizo za Kambini kichokochwe, Mchanga mdogo, Chwale na Mjini kiuyu, mradi huo, ulilazimisha kuanzishwa kwa kamati hizo.

Jambo zuri kwenye kamati hizo zenye lengo la kukabiliana na mabadiliko tabia nchi, sambamba na kujiongezea kipato, wanawake wapo 68 na wanaume na wanaume 33.

Hili ni jambo jema, kwa jamii na wanaouendesha mradi huo ambao ni Jumuia ya uhifadhi wa misitu Pemba ‘CFP’ wakishirikiana na wenzao wa kimataifa ‘CFI’ kwa ushirikiano wa karibu na TAMWA Zanzibar  kwa ufadhili wa  Serikali ya Canada, na kuridhiwa na Serikali ya Mapinduzi.

HAYA YALIKUJAJE KWA WANAWAKE KUWA WINGI

Bakar Hamad katibu wa kamati ya upandaji wa mikoko ya Kambini kichokochwe, anasema kamati yake  inawajumbe  55,  wanawake 31 na wanaume 24.

Anasema wanawake ndio wahanga wakubwa wa mabadiliko ya tabianchi, hivyo unapomuelimisha na kumpa nyenzo yuko tayari kuhakikisha anayatunza mazingira, ili awe salama.

‘’Yanapotokea mafuriko wanawake hua ndo wahanga wakubwa, na ndiomaana mradi ukalenga kwa wanawake  zaidi,’’anaeleza.


Fatma Shaaban Mohamed ni kiongozi wa kamati ya kilimo msito  Shehia ya Mjini kiuyu, anasema katika kamati yake ana wajumbe 25 wanawake 20 wanaume watano sawa na asilimia 0.05.

Anasema anampango wa kuongeza tena wajumbe wanawake kwani,  alishaona  kilimo msitu kitawasaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

‘’Ukilima kilimo mseto,  katikashamba hilo moja, utavuna mazao utakula, utauza, utapata kuni, na utaepusha mmon’gonyoko wa ardhi,’’anaeleza.


Anu Omar Juma ni kiongozi wa Kamati ya uhifadhi wa mazingira, inayojishughulisha na kilimo mseto ya Mchanga mdogo, ina wajumbe sita (6) wote ni wanawake.

Anasema hajashirikisha wanaume, kwani  anahisi athari za mabadiliko ya tabianchi, wathirika zaidi ni wanawake.

‘’Wanawake ndio wanaohangaika kutafuta kuni,hivyo wakilima kilimo msitu wataepuka  kukata miti kiholela, itakua wanazipata katika mashambayao,’’anaeleza.

Ali Juma Mbarouk kiongozi kutoka Chwale anasema kamati yake ya kilimo msitu, ina wajumbe 15 kati ya hao, wanawake ni 11 na wanaume ni wanne (4).

Anasema ameamua kuwashirikisha wanawake wengi, kwasababu wao ndio wanahitaji zaidi elimu ya mabadiliko ya tabianchi.

‘’Elimu ya mabadiliko ya tabia nchi inaweza kuinua kipato cha wanawake, kwani wanaweza kulima kilimo cha biashara na kujingizia kipato,’’anasema.

Asya Abeid Said  mwanakamati wa Mjini kiuyu, anasema siku zote panapokuwepo na kiongozi mwanamke ni rahisi kufanikiwa.

‘’ Kwa vile mradi huu umempa fursa kubwa mwanamke, naamini athari zitokanazo na uharibifu wa kimazingira zitapungua kwa kiasi kikubwa,’’anafafanua.

Bakar Amour nae ni mwanakamti ya Mchanga mdogo anasema, mradi wa mabadiko ya tabianchi, utawajenga wanawake, kua na uthubutu wa kushiriki katika nafasi yeyote ya uongozi.

‘’Walipoelimishwa na wakafahamu sababu za uharibifu wa mazingira, nasubutu kusema kumeundwa kamati hakuna anayeweza kukata mikoko,’’anasimulia.

Maryam Khamis Bakari mwenyeulemavu wa uziwi mwanakamati Mchangamdogo, anasema anapokuepo kiongozi mwanamke, hupatikana mabadiliko.

‘’Kunapotokezea tetemeko la ardhi, mafuriko na mimi yananikumba, ndio wakanishirikisha kwenye kamati yake ili niweze kufahamu mabadiliko ya hali ya hewa,’’anasema.

Mafunda Haji Khatib kutoka shehia ya Chwale anasema wameona faida ya kuwa na kiongozi mwanamke, kwani wengi shehiani mwao wamekua na mwamko wa kulima kilimo msitu.

‘’Tunashuru mwanamke mwenzetu kwa kutupa elimu ya utunzaji wa mazingira, na sasa tunapanda miti, ili tuweze kukabiliana nayo,’’anasema.

JAMII

Maryam Abdala Hamad mkaazi wa  Chwale amesema, kiongozi mwanamke ni bora, kwani mara nyingi ndio yuko karibu na jamii yake.

Kombo Khatib Bakar mkaazi wa Mjinikiuyu, anafahamisha kuwa, mwanamke ni mpenda mabadiliko, hivyo unampompa nyenzo anaweza kufanikiwa.

‘’Walipatiwa elimu ya utunzaji mazingira wanawake wachache, ila niseme wengi wao sasa hivi wametafuta mashamba wanalima kilimo mchanganyiko,’’anafafanua.


WANAHARAKATI

Hafidh Abdi  Said kutoka jumuiya ya  utetezi wa kimazingira  na jinsia Pemba ‘’PEGAO ’’ anasema  kwa baadhi ya tasisi tayari wamekuwa na uwelewa wa kuitekeleza Sera ya jinsia, kwani wanawashirikisha wanawake katika miradi ya kimaendeleo.

Nairat  Abdullah  Ali, kutoka Chama cha wandishi wa habari  wanawake  (TAMWA)    Zanzibar, anasema mradi huo wa uhifadhi mazingira, utainua kiapato cha wanawake sambamba na kuepukana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Mbarouk Mussa Omar Mkurugenzi wa Jumuiya ya uhifadhi wa misitu Pemba (CFP), anasema kupitia mradi huo wamewekeza  zaidi kwa wanawake, kwani athari ya mabadiliko ya tabianchi inawaumiza zaidi.

‘’Tunataka kila penye watu 100 basi 80 iwe wanawake ambao wanafahamu athari za mabadiliko ya tabianchi na jinsi kukuabiliana nayo,’’anafahamisha.

  VIONGOZI WA  DINI

Sheikh Said Ahmed Mohamed kutoka Ofisi ya Mufti Pemba anasema, uislamu umemruhusu  mwanamke  kushiriki katika fursa yoyote ya kimaendeleo,  anayoiweza kwa mujibu wa dini.

Mchungaji Yohana Ali Mfundo wa Machomane Chake chake, amefahamisha kuwa katika dini yao hakuzuiwa  mwanamke asishiriki kwenye miradi ya kimaendeleo.

NINI KIFANYIKE.

Sheha wa Kambini kichokochwe, Ali Omar Ali anasema,  ni vyema na miradi mengine ya maendeleo inayokuja  kuiga mfano huo,  kuhakikisha wanazingatia usawa.

Si jambo geni wanawake kuonekana wengi katika kamati hizo za uhifadhi  mazingira, kwani hata Sensa ya watu na makizi ya mwaka 2022  Zanzibar imeonekana kua na wanawake wengi dhidi ya wanaume

Lakini hata kwa shehia ya Mchangamdogo yenyewe inayo wanawake 2385 huku,  wanaume  wakiwa 2207 kamailivyo shehia ya Kambini kichokochwe inayowanawake, 2067 na wanaume 1938.







Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO