WAANDISHI WA HABARI MSHICHOKE KUDAI MABADILIKO YA SHERIA.
Na Fatma
Hamad- Pemba
Waandishi wa
habari wamehimizwa kuendelea kuzipigia kelele Sheria za habari ziweze
kurekebishwa, jambo litalopelekea kuondosha khofu na woga kwa wanahabari hao.
Akizungumza katika
mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo juu ya kufanya ushawishi na utetezi
kwa Sheria za habari, kwa wandishi wa vyombo mbalimbali vya habari, Afisa
programu kutoka Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar Zaina
Abdala Mzee, amesema ipo haja kwa wandishi wa habari kupaza sauti zao kwa kuzisemea
Sheria hizo, ili kuona kilio chao kimepatiwa ufumbuzi.
Afisa huyo ameyasema hao huko ukumbi wa Tamwa Chake chake Pemba, ambapo amesema endapo kilio cha wandishi wa habari kitazingatiwa na kupatikana kwa Sheria mpya za habari, kutasaidia wandishi wa habari kufanya majukumu yao bila ya khofu wala woga wowote.
‘’Kama
kutapatikana Sheria mpya ambayo itakua haina vifungu vinavyokwaza uhuru wa habari,
kutawasaidia wandishi kufanya kazi zao wakiwahuru,’’ameeleza.
Akitaja vifungu ambavyo vimekua ni kandamizi kwa wandishi wa habari, Mkufunzi wa Mafunzo hao Haura Shamte kutoka Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania [TAMWA] Zanzibar amesema ni kifungu cha 4, na kifungu cha 27[1] vya sheria ya Usajili wa wakala wa habari Magazeti na vitabu No 5 ya mwaka 1988 iliyo rekebishwa na sheria no. 8 ya mwaka 1997.
Ameendelea kusema kuwa vifungu vengine ambavyo vimekua ni
kikwazo kwa wandishi wa habari pamoja na vyombo vya habari ni kifungu cha 27
(1) na 27 (2) vya sheria ya Tume ya Utangazaji No. 7 ya mwaka 1997 kama
ilivyofanyiwa marekebisho na sheria No 1 ya mwaka 2010.
Aidha
ameendelea kusema kuwa wakati umefika
kwa wanahabari kufanya utetezi kwa kina
juu ya Sheria hizo, ziweze kufanyiwa marekebisho na kuona zinaendana na wakati.
‘’Kwa kweli
sheria yetu imeshapitwa na muda tunaomba ifanyiwe marekebisho ili kuondoa
vifungu ambavyo vinakinzana na uhuru wa vyombo vya habari, amesema.
Nao waandishi waliopata mafunzo hayo wameahidi kuendeleza mapambano ya kufanya ushawishi, ili kuona mamlaka zinazohusika na masuala ya Sheria, zinatimiza azma ya wandishi wa habari ya kupata Sheria mpya ambayo itakua rafiki kwao.
Comments
Post a Comment