Jumuiya za vyama vya siasa, muarubaini wa kuwasaidia wanawake kwenye uongozi

 


NA FATMA HAMAD, PEMBA

MWENYEKITI wa CUF  Mhamed Haji Kombo, wa Chake chake akiri kuwa uanzishwaji wa jumuia za wanawake ndani ya vyama vya siasa, zimesaidia kwani zimewaamsha wanaume kufahamu kwamba, haki ya kugombea ni kwa wanachama wote.

Aanasema jumuia za wanawake zimezaa matunda kwani wanawake katika Chama chao wamekua na uthubutu wa kugombea nafasi za ungozi, ambapo ngazi za kitaifa viongozi wengi ni  wanawake.

’ ‘Wamekuwa wakipata elimu na mafunzo mbali mbali  kwenye jumuia zao, na ndo maana wakawa na uthubutu huo wa kuhodhi nafasi za uongozi,’’ Amesema Mohamed wakati wa mahojiano.

Mwenyekiti wa Chama cha ACT WAZALENDO Mkoa wa Kusini Pemba kichama, Saleh Nassor Juma anasema mchango wa Ngome za Wanawake ni mkubwa kwani zimewafanya wanawake waondokanae na hofu ya kugombea na kushika nyadhifa za uongozi.

 ‘’Kwa kweli hizi Jumuia za wanawake kwenye vyaama zimewatoa hofu wanawake, maana ukiangalia kwenye kamati yetu ya  uongozi ya Mkoa Chake chake  takribani asilimia 50 ni wanawake, nahii ni kutokana na elimu wanayopatiwa,’’ ameeleza.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Wiala  ya Micheweni Khamis Juma Omar anasema lengo kuu la kuanzishwa kwa jumuiya za wanawake ni kuonesha umuhimu wa mwanawake na  kuona kwamba hawajaachwa nyuma katika harakati za kisiasa.

Amefahamisha kuwa wengi wa wanawake wamekuwa na ujasiri wa kujingiza majimboni na kugombea  hii ni kutokana na kuwanzishwa kwa jumuiya zao hizo za wanawake .

Khamis amesema jumuiya ya wanawake (UWT) ya chama chao wamekuwa wakipatiwa mikopo serikalini.

‘’Tumekua tukiwasimamia na kuhakikisha wanapata mikopo na mfuko wa uwezeshwaji wanawake kiuchumi ili kuona wanaendesha shughuli zao ambazo zitakazowsaidia katika harakati zao za uongozi,’’

Uwepo wa jumuia za wanawake ndani ya vyama vya siasa, ndio tenuri la wanawake, kujengewa uthubutu wa kugombea nafasi zilizoonekana ni za wanaume pekee.

WANACHAMA WA VYAMA VYA SIASA

Shaame Suleiman Shaame ni mwanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM mkaazi wa Sizini  Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, anasema anakumbuka katika wilaya yao ya Micheweni nafasi ya uwenyekiti kwenye Chama hicho ilishawahi kushikwa na mwanamke.

‘’Wanawake wanapatiwa uwezeshwaji wa mafunzo ili waweze kujiamini, pamoja na mikopo ya ujasiariamali kupitia kwenye Jumuia zao hizo za Umoja wa Akinamama,’’amemalizia.

Jumuiya za wanawake ndani ya vyama vya siasa hazipo tu kwa ajili ya kuvinufaisha vyama bali vimekua ni mkombozi mkubwa kwa wanawake.

Hili limethibitishwa na Tumu Mwali Masoud (40) ambae amelelewa na jumuia ya wanawake (UWT) ambapo kwasasa amekua na uthubutu wa kuingia jimboni na kugombea.

Tumu anasema jumuiya imemnufaisha kwani alishapata mafunzo mbalimbali yakiwemo ya Uongozi.

Anasema Katika uchaguzi uliopita wa 2020 aliingia kwenye uchaguzi na kugombea jimbo kwa upande wa uwakilishi,kwa vile alijiona anaweza kwani alikua tayari alishandaliwa na Chama chake.

’’Nililelewa na jumuia ya wanawake wa chama changu cha  Mapinduzi CCM, na ilinijengea uthubutu na mwaka 2020, niliingia jimboni na kugombea,’’ anasimulia Tumu.


Ziada Khalfan Saleh, (48) mwanachama wa Chama cha Tanzania Labour Party –TLP, anasema anapata semina za ndani na nje ya kisiwa cha Pemba, jambo linalomfanya kujuana na watu tofauti tofauti na  kubadilishana mawazo juu ya uongozi kwa mwanamke.

‘’Tunapelekwa  kwenye mafunzo ili tuweze kujiamini na kua Viongozi bora,’’amesema

ASHA Mohamed Ali, (45 ) mkaazi wa Wawi Chake Chake ambae ni mwanachama wa Chama cha United DemockratiC Party –UDP, aliejiunga  na jumuia ya wanawake tokea mwaka 2012.

 Amesema mchango wa jumuiya za wanawake ni mkubwa, na ndio sehemu ambayo kupitia jumuiya hizo, amepata nafasi ya  kuteuliwa kuwa Makamo Mwenyekiti wa UDP Mkoa wa Kusini Pemba.

‘’Jumuiya imenisaidia kwani baada ya kuonekana nafanya vizuri kwenye majukumu ya jumuiya, nimeteuliwa kupewa uongozi wa kwenye chama,’’Amesema Asha ambaye ameona fursa kuwa kwenye jumuiya hizo.

VIONGOZI WA JUMUIYA ZA WANAWAKE

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania – UWT Wilaya ya Micheweni, Mkitu Hassan Mwalim anasema katiba ya jumuiya yao, imetekelezeka kwa Chama cha Mapinduzi kimekua kikiwapatia ruzuku,pamoja na mafunzo ya uongozi.

‘’Binafsi nimeandaliwa kuptia jumuia nasasa nimekua kiongozi, na nawaelimisha wananchi wangu wanake ili nawao wawe na uthubutu wa kusimama popote na kzungumza, pamoja na kugombea,’’amesema.

Batuli Mussa Sharif, (46) Naibu katibu wa idara ya Uchaguzi (Oganazitio) Zanzibar kutoka Chama cha  ACT WZALENDO  mkaazi wa Kijichame  Wilaya ya Micheweni Pemba, amasema jumuiya kwenye chama chao jumuiya inaitwa Ng’ome ya wanawake ,amesema jumuiya hizo za wanawake  zimekuwa zikiwasaidia  kwani  wanapata mafunzo kuhusu kujiamini na kuondokana na woga.

‘’Binafsi baada ya kupata mafunzo nimeelimika na  nina uthubutu wa kusimama popote na nikazungumza, na najitayarisha mwakani kuingia kwenye jimbo kugombea,’’Amemalizia Batuli.

MWANAHARAKATI

Mwanaharakati wa masuala ya kupambana na haki za wanawake na watoto Wilaya ya ChakeChake Kisiwani Pemba Amina Omar Mselem,anasema ni  jambo jema uwepo wa jumuiya za wanawake kwenye vyama kwani wengi ambao wamekua na uthubutu wa kusimama mbele za watu na kujieleza ni wale ambao wamepitia kwenye jumuiya hizo.

‘’Kiukweli jumuiya zina mchango mkubwa kwani wengi wa wanawake ambao wanajingiza kwenye kinyanganyiro cha kuwania majimbo ni wale ambao wanatoka kwenye Ngome kwani elimu inakuwa inatolewa vya kutosha ili waweze kujiamini’’.Amemalizia Amina.

TAKWIMU

Takwimu za uongozi za vyama vya siasa zilizokusanywa mwaka 2024 na afisi ya msajili wa vyama vya siasa Tanzania, zimeonesha hadisasa kunavyama vitatu tu ambavyo wenyeviti wanawake ambavyoni CCM, ACT_ wazalendo na SAU.

Aidha kwa nafasi za Makatibu Wakuu pia nivyama vitatu (3 ) tu ndio vyenye Makatibu Wakuu wanawake ambavyo ni CCK, UNDP na NCCR_Mageuzi.

Kwa  Pemba ambako kuna Wilaya nne na Mikoa miwili, ni  vyama  vinne (4) tu,  ndivyo vinamakatibu  wanawake  wa  mikoa,  ambavyo ni, TLP, NRA, NLD  na CHAUMA .

Kwa mujibu wa ripoti Maalumu ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, iliyotolewa na Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake  Tanazania Zanzibar (TAMWA) imesema kuwa, nafasi ya uwakilishi kwenye majimbo 50 ya Zanzibar wanawake ni asilimia 16 ambao ni nane tu.

Kwa upande wa Ubunge wanaowakilisha Zanzibar wanawake ni, wanne sawa na asilimia 8, Mawaziri wakiwa ni sita sawa na asilimia 33 na Makatibu wakuu ni saba sawa na asilimia 39.

Kwa upande wa Wakuu wa Mikoa mwanamke ni mmoja tu sawa na asilimia 20, Wakuu wa Wilaya ni wanne sawa na asilimia 36 na Masheha wanawake 81 sawa na asilimi 20, kwenye shehia 388 ya masheha wote Zanzibar.

SERA YA CHAMA CHA MAPINDUZI

Sera ya Chama cha Mapinduzi ni kuongoza umma wa watanzinia katika ujenzi wa uchumi wa kisiasa utakaoleta maisha bora ya wananchi kwa kuwawezesha kiuchumi.

KATIBA YA (UWT) TANZANIA

Katiba ya jumuia ya umoja wa wanawake Tanzania –UWT ya mwaka 1978 toleo la mwaka 2017, imesema UWT itapata ruzuku kutoka Chama cha Mapinduzi.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO