Jamii yatahadharishwa kuachwa nyuma wanawake wenye ulemavu mradi mabadiliko tabia nchi
Na Fatma Hamad- Pemba
…...hana
mguu, hana mkono, haoni, atawezaje kutunza mazingira…….
HAYO
NI MANENO ya ALi Juma Mbarouk kiongozi wa kamati ya uhifadhi mazingira Chwale
anasema wanawake wenye ulemavu ni vigumu kuingizwa kwenye kamati za utunzaji
mazingira.
Anasema kamati yake, ina wajumbe 15, kati ya hao hamna
hata mjumbe mmoja mwanamke mwenye ulemavu.
Anasema hajamshirikisha
mwanamke yeyote mwenye ulemavu, kwani anadhani hawezi kufanya shughuli
hizo za uhifadhi kutokana na hali zao.
‘’Mtu aliekua hana mguu, hana mkono, wala haoni
atawezaje kupambana na mabadiliko ya tabianchi hasa kwa kuwemo ndani ya
kamati,’’anasema.
VIONGOZI/WAJUMBE WA KAMATI
Fatma Shaaban Mohamed ni kiongozi wa kamati ya kilimo
mseto Shehia ya Mjini kiuyu, anasema katika kamati yake anao wajumbe 25 mtu
mwenye ulemavu hana hata mmoja.
Anasema hajawahi kumpa elimu ya mabadiliko ya
tabianchi, mwanawake yeyote
wenyeulemavu.
‘’Kwakweli sijawatafuta wenye ulemavu nawao
nikawaingiza katika harakati hizi za utunzaji wa mazingira,’’anathibitisha.
Bakar Hamad kutoka kamati ya upandaji wa mikoko ya
Kambini kichokochwe ambaye, kamati yake inao wajumbe 55, kati ya hao hakuna mjumbe mwanamke hata
mmoja mwenyeulemavu.
Anasema alitoa elimu kwa wananchi wote, ingawa wanawake
wenye ulemavu hawakuitikia ipasavyo wito huo, juu ya kujiunga na kamati hizo za mabadiliko ya
tabianchi.
‘’Mabadiliko ya tabianchi yanaathi watu wote, ila
nashangaa sijui kwa nini wenzetu hawa wenye ulemavu
hawajajitokeza,’’anajiuliza.
Kamati, inayojishughulisha na kilimo mseto ya Mchanga
mdogo ambayo inaongozwa na Anu Omar Juma,
ndio kamati pekee na ya kupigiwa
mfano ambayo, imewashirikisha wanawake wenye ulemavu.
Anasema kamati hiyo inawajumbe sita (6) wote ni
wanawake, wawili wakiwa ni wenye ulemavu.
Aliamua kuwaelimisha wanawake wenye ulemavu wajiunge
katika kamati hizo, ili kuona nawao wanajiinua kiuchumi, kupitia shughuli hizo
za uhifadhi.
‘’Watu wenye ulemavu nawao wanauwezo wa kutunza mazingira,
ndio maana nikawashirikisha ili waweze kupiga hatua juu ya mabadiliko ya
tabianchi,’’anasimulia.
Asya Abeid Said
mjumbe wa kamati ya kilimo msitu shehia ya Mjini kiuyu, anasema wanawake wenye ulemavu, hawajashirikishwa
kwenye harakati za mabadiliko ya tabianchi.
‘’Kwa kweli wenzetu wenyeulemavu hatujawatendea haki,
ni lazima tujitafakari, kwani kunapotokea kiangazi, wao ndo waathirika
wakubwa,’’anafahamisha.
Chumu Mbarouk Omar
mjumbe wa kamati ya uhifadhi
mazingira shehia ya Kambini kichokochwe, anasema bado jitihada za
kuwashajiisha wanawake wenye ulemavu,
kujiunga na kamati hizo ni ndogo.
WANAWAKE
WENYEWE WENYE ULEMAVU
Mwajuma Kombo
ambae ni mwenye ulemavu wa uoni, mkaazi wa shehia ya Mjini kiuyu, anasema bado
hajashajiishwa kujiunga kwenye kamati za uhifadhi wa mazingira.
Anasema athari za mabadiliko ya tabianchi zinawaathiri
watu wote, sasa iweje kama kweli wameshirikishwa wakatae kutunza mazingira.
‘’Inapotokezea mvua, jua, sisi wanawake wenye ulemavu
tunaathirika kwa kiasi kikubwa, tunahitaji tupewe elimu ya mabadiliko ya
tabianchi, ili tuweze kukabiliana nayo,’’anafafanua.
Anaona hakuna mtu yeyote, anaekataa jambo lenye kuleta
tija, ingawa kwa eneo hili la kukabiliana na mabadiliko tabia nchi
wamesahauliwa.
Maryam Khamis Bakari mwenye ulemavu wa uziwi mjumbe
kutoka shehia ya Mchanga mdogo, anasema ameshirikishwa katika kamati ya kilimo
msitu, ili aweze kupambana na mabadiliko ya tabianchi.
Anasema licha ya ulemavu wake, amekuwa akifanya vizuri
kama wengine wasio na ulemavu, juu ya utunzaji wa mazingira.
‘’Tayari nimeshatayarisha shamba langu vya kutosha, na
sasa changamoto yangu ni mbegu tu, ili
niwe mtu wa mbele wa kukabiliana na hali ya hewa,’’anasema.
Anasema alifuatwa nyumbani kwake na kupatiwa elimu ya
mabadiliko ya tabianchi, na anasema amekua mstari wa mbele kuifanyia kazi elimu
hiyo.

JAMII
Asha Ali
Khamis mkaazi wa Mchangamdogo anasema wenye ulemavu wanauwezo wa kufanya kazi
na wanauwezo wa kujitegemea wenyewe kiuchumi,hivyo ipo haja nawao
washirikishwe.
Hamad Ali
Omar mkaazi wa Mjini kiuyu, anasema athari za mabadiliko ya tabianchi
zinawakumba watu wote, kwanini na wao wasishirikishwe wakaweza kuepukana nayo.
KAULI ZA
VIONGOZI WA SERIKALI JUU YA WATU
WENYE ULEMAVU
Mwenyekiti
wa Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu Bi Salma Saadat Haji, anasema Watu
wenye Ulemavu wana haki ya kushirikishwa katika nyanja zote kama raia wengine.
Hidaya
Mjaka Ali katibu wa Jumuia ya wanawakewenye ulemavu kisiwani Pemba anasema mikakati
yao, ni kuwashajiisha wanajamii kuwapa fursa, ili na wao washiriki katika
harakati zote.
WANAHARAKATI
Chama cha
Wandishi wa habari wanawake (TAMWA) Zanzibar kimekua ni mdau mkubwa wa
kuielimisha jamii kuacha ubaguzi dhidi ya watu wenye ulemavu, hasa katika
masuala ya mabadiliko ya tabianchi, Nairat Abdullah Ali anaeleza.
Saada Juma
Segeja ni Afisa kilimo mseto kutoka taasisi ya Uhifadhi Misitu Pemba (CFP) anasema lengo la mradi huo, ni kuona watu
wote, wanaelewa wa athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi.
‘’Tunataka
jamii yote inufaike na fursa hiyo ya utunzaji wa mazingira, kwani tatizo la
mabadiliko ya tabianchi ni kikwazo kwa watu wote,’’anaeleza Saada.
ATHARI
Aisha Abdala Juma Afisa utawala
kutoka Shirikisho la jumuia za watuwenyeulemavu Zanziba (SHUJUWAZA) Ofisi ya Pemba, anasema endapo watu
wenyeulemavu hawatopatiwa elimu ya
mabadiliko ya tabianchi, wanaweza kuwa chanzo cha uharibifu wa mazingira.
NINI KIFANYIKE
Nivyema watuwenyeulemavu
kushirikishwa katika fursa zinazokujanchini, ili nawao wapate kunufaika nazo
wasiachwenyuma, Hidaya Mjaka kutoka Umoja wa wanawake wenye ulemavu Zanziba
upande wa Pemaba anafahamisha.
Kutokana na mabadiliko ya tabaianchi
ambayo yameonekana kuiathiri kwa kiasi kikubwa jamii, Tasisi ya upandaji misitu Pemba (CFP) wakishirikiana
na wenzao wa kimataifa CFI kwa ushirikiano wa karibu na Tamwa Zanzibar, wakaja
na mradi wa miezi 30 wa uhiadhi
mazingira.
Mradi ambao unafadhiliwa na Ubalozi
wa Canada ikishirikiana na serikali ya
Mapinduzi Zanzibar, unatekelezwa katika shehia za Mkijini Kiuyu, Mchanga mdogo,
Kambini kichokochwe na Chwale katika Wilaya ya Wete Pemba.
Kwa upande wa wajumbe wa kamati hizo nne za
uhifadhi wa mazingira wapo 101, kati yao
watu wenye ulemavu ni wawili (2) tu,
ambapo ni sawa na asilimia 2 ya wajumbe wote.
Kamati
hizo ambazo
zina viongozi tisa (9) hakuna hata mwanammke mmoja, mwenye ulemavu
NYARAKA
Licha ya kuachwa nyuma kwenye kamati hizo, Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar imeweka muongozo maalum, ili maendeleo ya nchi yasiwaache
nyuma Watu wenye Ulemavu, kwa kuimarisha muundo wa taasisi ya Watu wenye
Ulemavu.
Eneo jengine ni uwepo wa sheria nambari 8 ya mwaka 2022 ya
Watu wenye Ulemavu Zanzibar, nayo kifungu cha 28 (e) kinaeleza kundi hilo,
linahaki ya kuishi kwa kujitegemea na kujumuishwa katika shughuli za kijamii,
kiuchumi na kisiasa.
Kimataifa, nako haki ya
kushiriki katika harakati za kimaendeleo, imeelezwa kwenye ibara ya 9 ya
mkataba wa kimataifa wa watu wenye ulemavu ulioridhiwa na Tanzania mwaka 2009.
Hata Katiba ya Zanzibar ya 1984 Kifungu cha 21 (3) kinaeleza, wazi kuwa, ‘kila
mzanzibari anayo haki ya kufanya kazi na anastahili fursa na haki sawa, kwa
masharti ya usawa ya kushika nafasi yoyote ya kazi na shughuli yoyote iliyoko
chini ya mamlaka ya Zanzibar’.
CHANZO MITANDAO
Ripoti mpya
ya Hali ya Hewa na Maendeleo (CCDR) kwa Tanzania iliyozinduliwa na Benki ya
Dunia (WB) imetaja hatua tano zinazoweza kuchukuliwa kukabiliana na athari za
mabadiliko ya tabianchi.
Moja wapo ni
kuwajengea uwezo na uelewa wa kukabiliana na hatari zinazotokana na mabadiliko
ya tabianchi wanawake na makundi mingine.
Comments
Post a Comment