Huuhapa mkakati wa vyama vya siasa, kuwandaa wanawake kuelekea uchaguzi wa 2025.
Na Fatma Hamad – Pemba
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
lililotolewa azimio Octoba 31 mwaka 2000
limesema kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi inazidisha demokrasia
ya nchi, uchumi, amani na utulivu.
Eneo jengine ni katiba ya Zanzibar ya 1984 katika
kifungu cha 21 (1) kinaeleza kila
mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika kufikia uamuzi
juu ya mambo yanayomuhusu mwanamke na
taifa lake.
Hata Sera ya Chama cha Mapinduzi kwenye mkakati wake, ni kuongoza umma wa
watanzania katika ujenzi wa uchumi wa kisiasa,
utakaoleta maisha bora ya
wananchi kwa kuwawezesha kiuchumi.
Kwa
mujibu wa Mkataba wa Kikanda wa Nchi za
Kusini mwa Afrika, uliotiwa saini mwaka
2008 kupitia kifungu nambari 13 cha mkataba huo, kinaelezea
kuwekwa mikakati madhubuti ya kuwawezesha wanawake kimafunzo
na kuwashajiisha katika nyanja mbalimbali za siasa.
Kimataifa,
ni asilimia 26.7 tu wanawake kote ulimwenguni ambao ni wabunge, huku asilimia
35.5 wakiwa katika nafasi za serikalini.Huku
asilimia 28.2 tu ya wanawake wanaoshika nafasi za kiutawala mahali pa
kazi.
Emma
Rubagumya mbunge na mwanakamati wa Kamati ya masuala ya jinsia katika Bunge la
Rwanda,anayewakilisha nchi yake katika
Mkutano wa 63 wa Kamisheni ya hali ya wanawake CSW,katika Makao Makuu ya Umoja
wa Mataifa mjini New York,anasema ushiriki wa wanawake katika maamuzi ya ngazi
zote imewaweka mahali pazuri!
Bi
Emma Rubagumya akizungumza nje ya mkutano huo anasema wanawake wanapokuwa wengi
katika ngazi za maamuzi, inakuwa
rahisi kujua matatizo hasa yanayowakabili wanawake.
Kwa
mujibu wa takwimu za hivi sasa nchi za Rwanda, Cuba na Bolivia, zinaongoza kwa
kuwa na wawakilishi wanawake zikiwa na zaidi ya asilimia 50.
VIONGOZI
WA VYAMA VYA SIASA.
Hassan Khamis mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi
CCM Wilaya ya Micheweni Kisiwani Pemba anasema mkakati wao ni kuhakikisha
wanawake wa chama chao wamekua na uthubutu wa kuingia majimboni na kugombea
nafasi za uongozi.
‘’Kwasasa
tunawapa mafunzo wanawake ambayo yanajikita zaidi kujiamini na
kujitambua, ili waweze kuondokana na woga,’’ anaeleza.
Khamis anasema furaha yao ni kuona wanawake
wameingia kwa wingi majimboni, na
kujichukulia nafasi mbalimbali za uongozi.
Abass Mohamed Khatib Mratibu wa Chama cha Demokrasia Makini (DP) kisiwani Pemba, anasema wanawapa elimu ya uongozi wanawake wa Chama chao, ili waweze kujiamini na kuweza kugombea nafasi nje na ndani ya chama.
‘’Tunawapatia mafunzo ya uongozi wanawke, ili kuona na wao uchaguzi
mkuu wa mwakani wanaingia kwa wingi majimboni na kujichukulia nafasi mbalimbali
za uongozi,’’anasema Abass
Kumbe mkakati hauko kwa CCM pekee bali hata kwa upande wa Chama cha ACT WAZALENDO nako kunaunguruma,
kwani kumeanzishwa miradi maalum, kwa
ajili ya kuwasaidia wanawake kujipatia kipato.
Saleh Nassor
Juma ni Mwenyekiti wa ACT WAZALENDO Mkoa wa Kusini Pemba kichama,
anaeleza kwa sasa mkakati wao mkubwa wameweka miradi maalumu ambayoitawapitia kipato, ili wamudu kuendesha
shughuli zao za uongozi.
‘’Tumeanzisha miradi midogo midogo ambayo itawasaidia
wanawake kujiandaa na shughuli za uchaguzi wa mwakani,’’ anasema katibu.
JEE HILI
LINA UKWELI WOWOTE/WANAWAKE WENYEWE
Rukia Abubakar
Mohamed mkaazi wa Machomane, Aligombea
nafasi ya uwakilishi Jimbo la ChakeChake, anasema Chama chao kimekua kikiwajengea uwezo kwa
kuwapa mafunzo mbalimbali ya uongozi.
‘’Kama si
chama ambacho kinatuandaa na kutufanya
tuwe na uthubutu, basi wengine wangeshindwa kuingia majimboni na kuwania nafasi
na wanaume’’,alisimulia Rukia.
Anasema Chama chao kimekuwa kikiwapika vya
kutosha na ndio maana yeye amekua na uthubutu wa kuingia kwenye mchakato na
kugombea.
‘’Tumekua tukipatiwa mafunzo mbalimbali ya
uongozi, na ndio maana wengine tukaweza kuingia majimboni kuwania nafasi za
uongozi na wanaume,’’anasimulia Rukia.
Mpaji Abass mkaazi wa Chakechake, mwanachama
kutoka Chama cha ACT WAZALENDO, anasema chama chao kimekua kikiwapa mafunzo ya
kuwa na uthubutu na kujiamini, ili waweze kugombea.
‘’Nimejiunga kwenye chama huu ni zaidi ya mwaka
wa 18, nimejengwa vya kutosha na kwavile
tayari nishakua na uwezo, uchaguzi wa mwakani naingia jimboni kugombea ubunge
jimbo la Chakechake,’’anasema.
JAMII
Bimize Othman Ali, 42 mkaazi wa Wilaya ya Micheweni Sizini anasema mwanamke ana umuhimu mkubwa katika
ngazi za maamuzi, kwani ndo anaejua
zaidi kero na shida zinazowakumba wanawake wenzake.‘’Tukiwa tumebakiwa
na siku chake za kuingia mwaka wa 2025,
nivyema viongozi wa vyama vya siasa kuhakikisha wanawajenga wanawake, waondokana
na hofu, jambo litalowasaidia kuingia kwa wingi majimboni “ anasema.
WANAHARAKATI
Wanaharakati wa masuala ya jinsia na utawala bora
wako mstari wa mbele katika kuwasaidia wanawake kwenye masuala ya wanawake na
uongozi,Hafidh Abdi Saidi kutoka Jumuiya ya Utetezi wa Kimazingira na Jinsia
‘’PEGAO ’’ anasema licha ya kuwa wanawake wamekua na mwamko juu ya uongozi, lakini bado
ipo haja kwa wanasiasa
kuongeza nguvu ya kuwaelimisha wanawake,
ili wawe na uthubu wa kuingia majimboni kwa wingi.
‘’Ni wakati kwa wanasiasa kuongeza bidii ya
kuwajenga uwezo wanawake, ili kuona uchaguzi wa mwakani idadi ya wanawake kwenye
majimbo imeongezeka,’’anafahamisha.
Afisa Mkuu wa mahusiano kutoka Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar -TAMWA Sophia Ngalaphi, anasema vyama vya saisa viweke mkakati malaum wa kuwasuka na kuwapika wanawake ambao wanania ya kugombea , ili wasivunjike moyo na badalayake waingie jimboni na kugombea.
‘’Furaha
yetu kama wanaharakati
ni kuona wanawake wameingia kwa
wingi majimboni, ili
kupata idadi kubwa ya wanawake katinga
ngazi za uongozi,’’anasema Sofia.
NINI
KIFANYIKE
Ili kuhakikisha wanawake wameingia kwa wingi majimboni nakugombea
nafasi za uongozi na wanaume, katika Uchaguzi wa 2025 ni vyema kwa vyama vya
siasa, kuwandaa mpango mkakati wa
kuwapika wanawake waondokane na khofu, amedai Juma Kombo mwananchi kutoka
Wingwi kisiwani Pemba anaeleza.
Kwa
mujibu wa Sensa ya watu na
makazi ya mwaka
2022 Zanzibar inawanawake wengi ambao ni 974,281
sawa na asilimia
51.6 kuliko wanaume,
ikiwa wao ni 915,492
sawa na 48.4 ambapo
licha ya uwingi
huo bado idadi kwenye
ngazi za maamuzi
ni kidogo.
Kati
ya hao, ni asilimia 21.14 tu kwa wanawake 71 waliojitokeza kugombea udiwani.
Kwa
nafasi ya uwakilishi wanawake waliogombea ni 251, wakiwemo wanaume 190 na
wanawake 61, ambapo walishinda wanaume 42 na wanawake nane (8) sawa na asilimia
16, wabunge walioshinda wanawake ni wanne sawa na asilimia 8,
Takwimu za uongozi za
vyama vya siasa zilizokusanywa mwaka 2024 na afisi ya msajili wa vyama vya siasa
Tanzania ,kwani, zimeonesha hadisasa kunavyama vitatu tu ambavyo wenyeviti wanawake
ambavyoni CCM, ACT_ wazalendo na SAU.
Aidha kwa nafasi za Makatibu
Wakuu pia nivyama vitatu (3 ) tu ndio vyenye Makatibu Wakuu wanawake ambavyo ni
CCK, UNDP na NCCR_Mageuzi.
Kwa Pemba ambako kuna Wilaya nne na Mikoa miwili,
ni vyama
vinne (4) tu, ndivyo vinamakatibu
wanawake wa mikoa,
ambavyo ni, TLP, NRA, NLD, na CHAUMA .
Comments
Post a Comment