Adaiwa kubaka mtoto wa miaka mitatu
Na Fatma Hamad - Pemba
MAHKAMA ya Mkoa iliyopo Wete Pemba imempeleka rumande Rashid Ali Hamad (31) mkaazi wa Kiuyu kipangani, anaedaiwa kumbaka mtoto wa miaka mitatu.
Baada ya mtuhumiwa huyo kupanda katika kizimba cha Mahkama hiyo, alisomewa shauri lake, na Mwendesha Mashtaka wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Heri Hassan Omar, ambapo alikataa kata kata.
Pp Heri aliambia Mahkama kuwa kwa vile mshitakiwa amekataa shitaka lake, nivyema kesi ikaghairishwa na ipangiwe sikunyengine kwa ajili ya kusikiliza mashahidi, kwani tayari upelelezi ulishakamilisha.
‘’Mheshimiwa Hakimu tunakuomba tuipange siku nyengine, kwa vile ushahidi umeshakamilisha, ili tuite mashahidi,’’alidai.
Nae Hakimu Zuwena Mohamed Abdulkadir alikubaliana na Mwendesha Mashtaka, ambapo kesi itarudi Mahkamani hapo Novemba 18 mwakahuu, huku akimtaka mtuhumiwa abakie rumande hadi tarehe hiyo.
Imedaiwa Mahkamani hapo mtuhumiwa huyo Sebtemba 11 mwaka huu katika kijiji cha Kiuyu kipangani alimbaka mtoto wa miaka mitatu, jambo abalo ni kosa kinyume na kifungu cha 108 (1), (2),(e) na 109 (1) vya sheria ya adhabu namba 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.
Comments
Post a Comment