Wananchi wahimizwa kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura


 

                          NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wananchi ambao wameshafikia sifa za kuwa wapiga kura wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha  katika uboreshaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura linalotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Wito huo  umetolewa na Makamo mwenyekiti wa Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi Jaji mstafu wa Mahkama ya Rufaa  Mbarouk Salim Mbarouk katika mkutano wa wadau wa Uchaguzi kuhusu uboreshwaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura, huko Makonyo Chake chake Pemba.

Amesema ili kufanikisha ipasavyo zoezi hilo ni vyema wananchi kushirikiana na tume huru ya uchaguzi,na kuhakikisha wenye sifa za kuwa wapiga kura wanajitokeza kujiorodhesha kwenye daftari hilo.

‘’Ndugu wananchi tufahamu Tume huru ya uchaguzi imeanza na zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura,hivyo tuhakikishe kila mwenye sifa anapata haki yake hiyo,’’alisema.

Alisema kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha Sheria namba Moja ya mwaka 2024, Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Madiwani na wabunge itahakikisha inamuandikisha  katika Daftari la kudumu la mpiga kura mwananchi yoyote wa Tanzania aliekosa sifa ya kujiandikisha kwenye Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar.

Alieleza kuwa kwa upande wa Pemba Tume inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 8,162 ikiwa ni ongezeko la asilimia 18 ya wapiga kura wapya45,643waliopo kwenye Daftari la kudumu la wapiga Kura.

Aidha aliendelea kusema kuwa jumla ya vituo 40,126 vya kuandikisha wapiga kura vitatumika katika uboreshaji wa Daftari mwaka huu wa 2024.

Alieleza kuwa kwa upande wa Tanzania bara kuna jumla ya vituo 39,709, ikiwa Zanzibar ni 417, ambapo kuna ongezeko la vituo 2,312ikilinganishwa na vituo 37,814 vilivyotumika mwaka 2019/2020.

Aidha aliwasihi viongozi wa vyama vya siasa kuepuka kuingia katika  vituo vya kuandikisha ili kuepusha vurugu wakati wa zoezi hilo.

‘’Niwaombe ndugu viongozi kama kutatokezea tatizo basi ni vyema mkafuata njia sahihi kwa ajili ya kwenda kupeleka malalamiko yenu, na sio kuingia kwenye vituo ya uandikishaji,’’alieleza kwa msisitizo.


Mapema akiwasilisha mada ya uboreshaji wa Daftari la mpiga Kura Kaimu mkurugenzi wa Uchaguzi Giveness Nswile alisema kwa mujibu wa kifungu cha 10 cha sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani sheria namba moja ya mwaka 2024 miongoni mwa wananchi ambao hawana sifa za kuandikishwa katika Daftari hilo ni mtu asie na akili timamu, pamoja na asiekua raia wa Tanzania.

Kwa upande wake Balozi Omar Ramadhan Mapuri aliwasisitiza wadau walioshiriki mkutano huo kuwa mabalozi wa kuwaelimisha jamii kuhakikisha wanajitokeza kwenye  Daftari hilo ili waweze kuja kupata fursa yao ya kuwachaguwa Viongozi wanaowataka hapo mwakani.

Nao washiriki wa mkutano huo wameihakikishia Tume huru ya Taifa kutoa elimu kwa jamii na kuhakikisha kila mwenye sifa anapata haki yake hiyo.

Kauli mbiyu ya zoezi hilo la uboreshaji wa Daftari kujiandikisha  kuwa mpiga kura ni msingi wa Uchaguzi bora. 



     

 

 

Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO