Wanafunzi wapewa mbinu ya kujikinga na udhalilishaji




                                              NA SALIM HAMAD,  PEMBA 
Wanafunzi wametakiwa kutoa tarifa kwa watu wao wa karibu wakati wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji ili kuweza kujulikana na kuchukuliwa hatua.

Hayo yamesemwa na Msaidizi wa Sheria shehia ya Tumbe mashariki wakati akizungumza na wanafunzi wa Skuli ya Shumba vyamboni katika mkutano malummu ulioandaliwa na Jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Micheweni Pemba.

Alisema vitendo vya udhalilishaji hufanyika kila sehemu ikiwemo Madrasa, Skuli,Majumbani,hivyo ni budi kutoa tarifa wakati watakapofanyiwa.

‘’Msiyafiche matendo ya udhalilishaji hata kama mmefanyiwa na watu wenu wa karibu akiwemo mwalimu,kaka Mjomba toeni tarifa msione aibu’’,alisema.



Mapema msaidizi wa sheria shehia ya Tumbe Mashariki Fatma Hamad Faki aliwasisitiza wanafunzi hao wasipoke zawadi ya aina yoyote wanazopewa na watu ambao si wazazi wao ili kujikinga na vitendo vya udhalilishaji.

‘’Niwaombe ndugu zangu msishawishike na wala msipoke vizawadi mnavyopewa na watu ambao si maharimu zenu ni hatari  jiepusheni’’,aliwasisitiza.


Kwa upande wake Said Salim Khamis msaidizi wa sheria shehia ya Msuka aliwanasihi wanafunzi hao kushughulikia masomo yao kwanza ili waweze kufikia ndoto zao za badae.


Nae mwalimu anaeshughulikia kambi ya wanafunzi hao Seif Khamis amewashukuru watendaji wasaidizi wa sheria hao kwa kufika katika Skuli yao na kuwapatia elimu hiyo ya masuala ya udhalilishaji kwani inaweza ikawa dawa na kuogopa kufanya  vitendo hivyo.

 


 

 

  

Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO