Wakulima waikumbusha jambo Serikali
Wananchi
kisiwani Pemba ambao walikatiwa mikarafuu yao kwa ajili ya kupisha miundombinu
ya umeme wameiomba Serikali ya Mapinduzi kuwalipa fidia zao wakulima hao.
Wakizungumza
katika hafla ya ugawaji wa zawadi kwa washindi wa Vuna na Tigo pesa mkulima
Khamis Juma Khamis na Halima Mohamed Seif huko Makonyo Chake chake Pemba walisema
walikatiwa mikarafuu yao na kuahidiwa kulipya ila hadi leo hakuna chochote
walichokipata.
Walisema kuwa
karafuu ndio zao kuu wanalolitegemea kujipatia kipato, hivyo ni vyema Serikali
kulikalia kitako na kuhakikisha wanalipatia ufumbuzi suala hilo.
‘’Tulikatiwa
Mikarafuu yetu na tukaahidiwa tutalipwa ila hadi sasa hakuna lolote
tulilolipata’’,walisema.
Mapema
mkulima Ali Kombo Hamad alisema katika msimu wa karafuu ujao ni vyema shirika
la biashara la ZSTC kuboresha miundombinu ya kiwanda cha kununulia Makonyo
kilichopo wawi, kuhakikisha kinafanya kazi ili kuwaondoshea usumbufu wananchi
wanao kuja kuuza makonyo yao.
‘’Tulichukuliwa
viwanja vyetu kwa ajili ya kujengewa kiwanda cha kuzalishia Mafuta ya Makonyo
ila tunaona hakina faida yoyote, tunahangaika,’’pakuzia makonyo yetu,’’alisema.
Kwa upande
wake Ali Juma Ali alilitaka shirika la Biashara la ZSTC kuhakikisha wanapogawa
Mikarafuu kwa wakulima kuwapatia miche ya kutosha ambayo itawafanya waweze
kuotesha na kuzalisha kwa wingi.
‘’Unaweza
ukapanda mashina 15 ikaweza kuota mitatu, hivyo tunaomba mnapotoa msitupe miche
kidogo,’’alidai
Nae waziri
wa Biashara na Viwanda Zanzibar Omar Said Shaban aliwatoa hofu wakulima hao huku akiwahidi kulipwa fidia zao
ndani ya mwaka huu wa 2024.
Comments
Post a Comment