Posts

Showing posts from July, 2024

Dawa za kulevya zamsababishia kwenda Jelamiaka 7

Image
                                               NA FATMA HAMAD,PEMBA Ridhwan Mkongwe Sharif mwenyeumri wa miaka 38 mkaazi wa Kipange Konde Pemba,ameanza maisha mapya katika chuo cha Mafunzo kwa muda wa miaka saba, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kupatikana na misokoto 50 ya dawa za kulevya aina ya bangi yenye uzito wa gramu 210.5. Mapema Hakimu wa Mahkama ya Mkoa Wete Zuwena Mohamed Abdulkadir alisema, baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili na kuona kwamba hauna chembe ya shaka, mahakama imemtia hatiani mshtakiwa huyo. ‘’Kutokana na ushahidi uliotolewa na mashahidi wetu tumejirisha na kuona ushahidi uliotolewa ni wa ukweli hivyo mahkama imekukuta na hatia   mshitakiwa,’’ alisema. Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka D...

RUSHWA MUHALI BADO YAENDELEA KUOTA MZIZI KATIKA JAMII

Image
      NA FATMA HAMAD,PEMBA Mwakilishi wa Viti malumu Mkoa wa Kaskazini Pemba Hindi Hamad Khamis amewataka Wananchi wa Micheweni kuwacha tabia ya kuyafumbia macho matukio ya udhalilishaji jambo linalochangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa matendo hayo katika Jamii. Mwakilishi huyo aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Chamboni Micheweni Pemba katika mkutano maalumu ulioandaliwa na Jumuia ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Micheweni wa kutoa elimu kwa Jamii juu ya masuala ya udhalilishaji kwa wanawake na Watoto. Alisema bado wapo baadhi ya watu wanaendelea na tabia ya rushwa   muhali   juu ya matendo ya udhalilishaji, kwa kukhofia ugomvi katika familia zao, jambo linalowafanya   watoto kuishi kwa wasi wasi. ‘’Niwaombe wananchi wenzangu wa micheweni tuache muhali tusiogope unapodhalilishiwa mwanao toa mashirikiano katika vyombo vya sheria hata kama ni jamaa yako usifiche,alisisitiza’’ Alifahamisha kuwa Mkoa wa Kaskazini Pemba bado hali ya ...

ZAFELA YAWATAKA WAZAZI KUWARUHUSU WATOTO WAO WA KIKE KUSHIRIKI MICHEZO

Image
                        NA MARYAM SALUM,PEMBA JUMUIA ya Wanasheria Wanawake Zanzibar ZAFELA imesema imejipanga kuendeleza mapambano dhidi ya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia kwenye makundi ya michezo. Hayo yalisemwa na Rufea Juma kutoka Chama cha Wanasheri wanawake ‘’ZAFELA’’ Zanzibar   wakati akizungumza na asasi za kiraia pamoja na tasisi za Serikali katika mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya umuhimu wa michezo kwa mwanamke na mtoto wa kike yaliofanyika Gombani Chake chake Pemba.  Alisema kuwa lengo la kufanya hivyo ni kuona kunakuwepo na usawa wa kijinsia kwa jamii katika suala zima la michezo.  Alisema kuwa ingawa kumekuwa na dhana nyingi potofu kutoka kwa baadhi ya watu kudhani michezo kwa mtoto wa kike na mwanamke ni uhuni. ‘’Jamii imekua na dhana mtoto wa kike akishiriki michezo atakua muhuni, hali inayopelekea kukosa fursa za kimaendeleo zil...

MSHITAKIWA WA SHITAKA LA ULAWITI APATA DHAMANA

Image
      NA FATMA HAMAD, PEMBA MAHKAMA ya MkoawaKaskazini Pemba imempadhamana mtuhumiwa Faki Hamad Faki 35 mkaazi wa Kambini Mchangamdogo anayakabiliwa na mashitaka ya kutorosha na kumlawiti   mtoto wa kiume   mwenye umri wamiaka 12. Hakimu wa mahakama hiyo Zuwena Mohammed Abdalla alisema mahakama imeamua kumpa dhamana mtuhumiwa ni kutofika kwa mashahidi mahkamani kwa ajili ya kutoa ushihidi dhidi ya shaurihilo. Alifafanua kuwa kwa, mujibu wa kifungu cha 152 cha sheria namba 7 yamwaka 2018, sheria ya jinai inaeleza kwamba kama hakuna shahidi yoyote aliyefika mahakamani na kutoaushahidi kwa muda wa miezisita , mtuhumiwa apewe dhamana. “Kutoka na na kifungu hicho, Mahkama inampa dhamana mtuhumiwa    kwa masharti ya     shilingi laki tano taslimu   na wadhamini   wawiliwakiwa na kopi zakitambulisho cha Mtanzania au Mzanzibar, naakishiwa mtuhumiwa atarejea rumande” alieleza. Mapema mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka Ofi...

UBAKAJI BADO WAENDELEA KUWATESA WATOTO

Image
                                 NA FATMA HAMAD, PEMBA Familia moja Micheweni Pemba yakumbwa na huzuni kufuatia mtoto wao wa miaka mitano (5) kufanyiwa kitendo cha kuingiliwa kinyume na maumbile. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mama mzazi wa mtoto huyo huko nyumbani kwake alisema mtoto wake huyo   alifanyiwa kitendo hicho wakati alipokua shambani akiinga mtama. Alisema baada ya kurudi nyumbani kwao   mtoto alikua anatetemeka na kumuambia mama yake kuwa kuna mtu alimchukuwa na kumfanyia kitendo kiovu. ‘’Nilipo muhoji alinimbia kuna mtu kanichukua kaningiza kwenye boma na kunivua nguo na kunifanyia udhalilishaji,alisema’’mama mtoto. Alisema baada ya hapo walikwenda Hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi hatimae alionekana tayari ameshaathirika. Kwa upande wake baba mzazi wa mtoto huyo alisema kit...

MIDIPAO YAIKUMBUSHA JAMII

Image
                                                           NA FATMA HAMAD, PEMBA Jamii imetakiwa kurejesha malezi ya pamoja katika kuwalea watoto wao jambo ambalo litasaidia kuwakinga na vitendo viovu ikiwemo udhalilihaji. Ushauri huo umetolewa na Msaidizi wa sheria wilaya ya Micheweni (MIDIPAO) Ali Khatib Hassan wakati akizungumza na wananchi wa Chamboni Micheweni kisiwani Pemba. Alisema licha ya mikakati mbali mbali inayofanywa ili kuondosha udhalilishaji, lakini bado suala hilo   linaendelea kuwatesa watoto,hivyo ni vyema wazazi kushikamana katika malezi na kila mmoja kuumwa na mtoto wa mwenzake ili kuwalinda na vitendo hivyo. ‘’Kila mzazi na mtoto wake, hata ukimuona wa mwenzako anafanywa k...

Ni ipi nafasi ya familia katika kuwashajiisha watoto wa kike kushiriki michezo.

Image
Na, Fatma Hamad NA FATMA HAMAD, PEMBA Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kupitia idara yake ya michezo, imekuwa ikitoa fursa mbali mbali za kimaendeleo ikiwemo ajira, kushiriki mabonanza nje ya Zanzibar. Hilo limekuja kwa wazazi kutokuwapa nafasi watoto wa kike kushiriki michezo, kwani bado wanahisi kwa mwanamke ni uhuni na kupelekea siku zote kubaki nyuma kimichezo. Licha ya Serikali kutoa fursa nyingi za kimaendeleo, bado ushiriki wa wanawake na watoto wa kike, ni mdogo ukilinganisha na wanaume hapa visiwani Zanzibar, hususan kisiwa cha Pemba. Wazazi na walezi wanayo kila sababu ya kuhakikisha wanawapa nafasi (fursa) watoto wa kike, kushiriki kwenye michezo ili kuona nawao wanajinyakulia fursa zilizomo kwenye Sekta ya michezo. Kwani wapo wengi wamekuwa ni wachezaji wazuri wakati wanapokuwepo skuli, wanapomaliza vipaji hivyo hupotea. Makala hii itangazia nafasi ya wanajamii (familia ) katika kuwashajiisha watoto wa kike, kushiriki ipasavyo kwenye michezo. WATOTO Mtoto F...