WANANCHI WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUPATA MATIBABU
NA FATMA HAMAD,PEMBA
Wananchi wa mkoa wa Kaskazini Pemba
wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika kambi ya uchunguzi na matibabu iliyopo
Micheweni uwanja wa kwa mshaame mata, ili waweze kuchunguzwa na kujulikana
matatizo yao na kupatiwa tiba.
Wito
huo umetolewa na mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib wakati
akizungumza na wananchi wa mkoa huo
katika uzinduzi wa kambi ya Uchunguzi na Matibabu iliyoandaliwa na tasisi ya
Zanzibar Maisha bora Fondation huko Micheweni Pemba alisema matibabu hayo yatatolewa
bure kwa wanachi wote.
Alisema
lengo la Serikali ya Mapinduzi ni kuona
wananchi wanaishi wakiwa na afya njema,
hivyo ni vyema kila mwenye matatizo kufika katika kambi hiyo ili aweze
kuchunguzwa na kupatiwa huduma bora za afya.
‘’Taifa
bora linajengwa na jamii iliyo bora, hivyo msione tabu kuja kupata tiba kwani
ni bure,’’alisema
Alisema
endapo kama kutakuwa na wagonjwa watashindikana kupatiwa matibabu, katika kambi
hiyo watapewa rufaa na kwenda kutibiwa sehemu nyengine.
Aidha
kwa upande mwengine aliwataka wananchi hao kufanya mazoezi kwa wingi ili
waimarishe afya zao, na waondokane na maradhi nyemalezi.
Kwa upande wake Afisa mtendaji mkuu wa tasisi ya Zanzibar Maisha bora Fondation Fatma Fungo alisema katika mikoa ya Kaskazini ya visiwa vya Zanzibar imegundulika kuwa takriban asilimia 48 ya wanawake wenye umri wa kubeba ujauzito wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya lishe duni, hali ambayo inaleta athari kwa mtoto anaezaliwa.
‘’Kambi
hizi tumeziweka zaidi katika mikowa ya kaskazini ili kutatua tatizo hilo la
lishe katika mikoa hiyo,’’alisema
Alisema
mwenyekiti wa tasisi hiyo Maryam Mwinyi alisema atahakikisha anapambana na
changamoto hiyo ya lishe ili kuona hakuna
mtoto anaezaliwa na udumavu.
Afisa mdhamini wizara ya afya Pemba Khamis Bilali Ali alisema katika kipaombele cha wizara ya afya ni kuona wanaboresha huduma za afya ya msingi kwa wananchi wote.
‘’Tumejipanga,
Kutoa huduma bure, kuanzia kwenye vipimo na madawa,’’alisema.
Aidha
aliwata wananchi kujitokeza kwa wingi katika uchangiaji wa damu sama, kwa ajili
ya kuisaidia jamii.
Katika kambi hiyo jumla ya watu 50 wanatarajiwa
kupatiwa matibabu ya maradhi mbali mbali ikiwemo Saratani ya shingo ya mlango
wa kizazi, Saratani ya matiti, huduma za afya ya mama na mtoto, macho, Koo,
Pua, upimaji wa vipimo vya kimaabara, huduma rafiki kwa vijana pamoja na chanjo
ya Uviko 19.
Comments
Post a Comment