UVCCM YAOMBA KUFUNGIWA KWA MTANDAO WA KIJAMII WA X
NA FATMA HAMAD,PEMBA.
Umoja wa vijana (UVCCM) Mkoa wa Kaskazini Unguja umeiyomba Serekali ya Jamhuri ya Muungano na ile ya Zanzibar,kuuchukulia hatua mitandao ya kijami X (TWITTER) ikiwemo kuufungia ambao wamedai unakwenda kinyume na madili ya vijana wa Tanzania.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Ismail Ali Ussi alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Mjini Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba.
Alisema Serikali inapaswa kuangalia kwa karibu na kuufungia mtandao huo kawani unatoa maudhi ambayo si mazuri kwa Vijana wa Taifa hili wakihofia kuaharibika kwa Vijana.
Alisema mtandao huo unaweza kupelekea kuporomoka kwa madili ya vijana wa taifa hili kutokana na video zinazo rushwa na mtandao huo zinazoenda kinyume na madili .
Alisema mtandao huo kama huukuangaliwa unaweza kuleta taharuki na kusababisha kuwepo migogoro kwa Vijana hivyo wameomba Serikali kuchukua hatua za kuufungia.
‘’Tunaiyomba Srikali ya Jamhuri ya Muungano na ile ya Zanzibar,kuchukua hatua za kuufungia mtandao wa x kwani unakwenda kinyume na maadili ya Vijana wa Tanzania’’alisema.
Hata hivyo aliwataka Vijana kuwa makini katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii kwa kutojihusisha kurusha vitu ambavo havina nafafasi kwenye Jamii.


Comments
Post a Comment