WASAIDIZI WA SHERIA PAMOJA NA WANDISHI WA HABARI WAOMBWA KUJIKITA VIJIJINI NA KUIBUA KERO ZA WANANHI.
Akizungumza
katika hafla ya ufungaji wa mafunzo ya siku nne, yaliyo washirikisha
wandishi wa habari , watetezi wa haki za binadamu na wadau mbali mbali Siti
Habibu Mohamed kutoka afisi ya shirika
la msaada wa kisheria Pemba
(ZALHO)alisema ni wajibu wa wandishi wa habari kuibua na kutetea masuala ya uvunjifu wa haki za
binadam katika jamii ili ziweze kueleweka na kupatiwa ufumbuzi.
Alisema
kuwa, wandishi wa habari na watetezi wa haki za binadamu wana kazi kubwa katika kuibua na kutetea masuala ya uvunjifu wa haki za binadamu
katika jamii kutokana na uelewa mdogo wa wanajamii.
Alieleza
kuwa, kuwepo kwa shirika la msada wa kisheria kutawawezesha wananchi kuzifahamu haki zao na kuwa na
uthubutu wa kuzitetea pale watakapoona zimevunjwa.
Nae Afisa
habari kutoka Chama cha wandishi wa habari Wanawake
Tanzania (TAMWA) ofisi ya Pemba Gaspa
Charles alisema kuwa endapo wandishi wa
habari watandika na kuripoti habari kwa kuzingatia miko na madili ya kazi yao
itaepusha kuandika habari zenye migogoro katika jamii.
Nao
baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo walisema mafunzo hayo yatawasaidia katika
kutatua masuala ya uvunjifu wa haki za binadamu katika jamii zao.
Mafunzo
hayo yaliyoandaliwa na mwavuli wa asasi za kiraia Pemba,(PACSO) yaliwashirikisha wandishi wa habari , wadau
na watetezi wa haki za binadamu
yamedhaminiwa na UNDP.



Comments
Post a Comment