WANDISHI WA HABARI WAKUMBUSHWA KUANDIKA HABARI ZINAZO HUSU HAKI ZA BINADAMU
NA FATMA HAMAD, PEMBA`
WANDISHI wa
habari wametakiwa kuwandika na kuripoti habari zinazohusu masuala ya haki za Binadamu, ili
jamii ifahamu haki
zao, wajibu wao, na kuweza kuzitetea pindi wakiona zimevunjwa.
Ombi hilo limetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa shirika la
mtandao wa asasi za kiraia Pemba [Pacso] wakati akifungua mafunzo ya
kuwahamasisha wandishi kuandika habari zinazo husu masuala ya haki za
binadamu yaliyofanyika Ranzi Vitongoji
Chake chake.
Alisema wandishi wa habari wana nafasi kubwa katika
kuielimisha jamii, hivyo ni budi kuwaelimisha kwa kuandika habari zinazogusa
haki za binadamu, ili waweze kufahamu haki zao, wajibu wao na kuweza kuzisemea.
‘’Tunawaomba Wandishi muchukuwe jitihada za makusudi
kuielimisha jamii kwa kuandika na kuripoti habari zinazo husu haki za binadamu, ili waweze
kuzifahamu na kuweza kuzitetea ,’’alisema.
Akiwasilisha mada juu ya haki za binadamu Mwanaharakati kutoka
shirika la Msaada wa Kisheria Pemba [ZALHO]
Siti Habibu Mohd alisema miongoni mwa haki za msingi ambazo anatakiwa azipate
binadamu ni kama vile Elimu, Kupiga kura, Matibabu pamoja na kumiliki mali.
Alisema endapo
wandishi watandika ipasavyo masuala ya haki za binadamu pale watakapona
zinavunjwa kutapelekea kuchukuliwa hatuwa
na kuweza kutatuliwa kwa haraka.



.jpg)
Comments
Post a Comment