WAKULIMA WAIOMBA SERIKALI KUONGEZA BEI YA MWANI.


NA FATMA HAMAD, PEMBA

WAKULIMA  wa  kilimo  cha Mwani  kisiwani Pemba  wameiomba   Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar  kuwangalia  tena   kwa jicho  la  huruma, kwa  kuongeza  bei  ya  mwani.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi  mkulima Raya Salim Faki kutoka Mjini Kiyu amesema bei ya mwani ya kilo shilingi 1000 bado ni ndogo, ukilinganisha na gharama wanazozitoa wakati wa kulima.

Alisema  dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya awamu ya Nane ni kuwaimarisha wakulima wa Mwani kichumi, hivyo ni wakati kuongeza bei hadi shilingi 3000.

 ‘’Bei ya shilingi 1000 haikidhi haja, kwani Tunanunua Kamba pamoja na taitai kwa gharama kubwa,hivyo tunaiomba Serikali ituengezee bei, ifike angalau elfu 3000,’’ alisema.

Kwa upande wake mkulima Salim Mbarouk Haji alisema  bado wakulima wa mwani hawajanufadika na zao hilo, kwani kilimo hicho kina changamoto nyingi.

 ‘’Kiukweli hasa tusifichane wanaonufaika na zao la mwani ni makampuni yanayo nunua mwani na sio wakulima,  wakulima wanaishia kunyanyasika tu,’’ alieleza.


Nae Hadia Hamad Ali alisema  asilimia 80 ya wakaazi wa Mjini kuyu wanategemea kilimo cha mwani kuendesha maisha yao, hivyo ipo haja kwa  Serikali  kufikiria kuongeza bei.

Aidha alisema wanakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa vitendea kazi ikiwemo Boti za kuchukulia mwani.

‘’Tunasikia tu kama kuna boti za mkopo ila sisi hatujazipa, hivyo tunawaomba wahusika watufanyie msada na sisi watupatie tunateseka,’’alieleza.


Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Mwani ya Serikali [ZASCO] Masoud Rashid Muhamed alisema kuwa bei ya mwani itaongezeka  mara baada ya kumalizika  ujenzi wa kiwanda cha mwani Chamanangwe.

Alisema  wanatarajia kuanzia June mwakani kiwanda hicho kitanza uzalishaji wa bidhaa  zinazotokana na mwani, hivyo wakulima watapata fursa ya kuuza bidhaa hiyo kwa bei nzuri.

Alisema  kiwanda hicho kitakua na uwezo wa kuchakata  tani zaidi 30,000 za mwani kwa mwaka, hivyo kuendelea kuvumilia.



Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO