KATIBU MKUU AHIDI KUSHUSHA NEEMA KATIKA SEKTA YA ELIMU
NA FATMA HAMAD, PEMBA
KATIBU mkuu wizara ya Elimu na
mafunzo ya amali Zanzibar Khamis Abdala Said amesema wizara itahakikisha
inaboresha mazingira rafiki kwa walimu, pamoja na kuwapatia haki zao stahiki,
ili wawe na hamu ya kusomesha, na kuleta ufaulu mkubwa kwa wanafunzi.
Katibu huyo
ameyasema hayo kwa niaba ya Warizi wa Elimu na mafunzo ya amali
Zanzibar Lela Muhamed Mussa wakati akifungua Kongamano la walimu ikiwa
ni shamra shamra ya kuelekea siku ya madhimisho ya walimu duniani, huko Chuo
kikuu cha Taifa Suza kilichopo Mchanga mdogo wilaya ya Wete kisiwani Pemba.
Amesema ni
haki ya kila mwalimu kuhakikisha anapata stahiki zake ambazo anatakiwa
kuzipaga.
‘’Tutashirikiana
bega kwa bega na chama cha walimu ili kuona changamoto zinazo wakwaza walimu
zimeondoka,’’alisema.
‘’Naishauri
Serikali ifanye mchakato wa kuwanzisha
Tume hiyo kwa haraka iwezekanavyo, ili kuona walimu wananufaika na tume hiyo na
kuondokana na changamoto zinazo wakabili,’’alieleza.
Alisema kuwepo
kwa tume ya utumishi ya walimu ni jambo jema, kwani kutapunguza changamoto
zinazowakwaza walimu pamoja na kuepusha mianya ya kuwepo kwa mishahara hewa.
Hivyo amewataka walimu wakuu kusimamia vyema majukumu yao na kuhakikisha wanafunzi wanafanya vizuri katika mitihani yao.
![]() |






Comments
Post a Comment