KAMISAA WA SENSA AWAPA DARADA VIONGOZI WA SERIKALI
KAMISAA wa
Sensa ya watu
na makazi ya
mwaka 2022 Tanzania
Zanzibar Balozi Mohammed
Haji Hamza amezitaka Tasisi za
Serikali kuzitumia Takwimu za Sensa
katika kupanga mipango kazi ya
shughuli zao za kimaendeleo.
Balozi huyo
ameyasema hayo wakati akuzungumza na Viongozi na mafisa mbali mbali wa Serkali
katika mkutano wa uhamasishaji wa matumizi ya matokeo ya Sensa huko Ukumbi wa
Baraza la Wawakilishi Wete mkoa wa Kaskazini Pemba.
Amesema
endapo watazitumia takwimu za Sensa ipasavyo kutawawezesha kuendesha vizuri
mipango yao ya kimaendeleo, hivyo ni wakati kwa Tasisi kuzifahamu Takwimu hizo
na kuzifanyia kazi.
‘’Ni vyema
yinyi viongozi kuhakikisha mnazipata kwa usahihi takwimu za Sensa na kuzifanyia
kazi katika tasisi zenu, ili ziweze kuwasaidia katika mipango yenu,’’alisema.
Samba mba na
hilo aliwaomba viongozi hao kuzifikisha takwimu hizo katika jamii, ili nawao
waweze kuzifahamu na kuzitumia katika kuendesha maisha yao.
Nae mkuu wa
wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya amesema takwimu hizo zitawawezesha kujua
changamoto zilizomo katika maeneo yao, huku akiahidi kutowa elimu kwa jamii ili
nawao waweze kuzifahamu.



Comments
Post a Comment