JAMII YATAKIWA KUWACHA TABIA YA KUWABAGUA WATU WENYE ULEMAVU

SALIM HAMAD,PEMBA

MKUU  wa Wilaya ya Mkoani  Khatib Juma Mjaja,  amewataka wananchi  kuacha tabia ya kuwafungia ndani watu wenye ulemavu kwani kufanya hivyo kunawakosesha haki zao za msingi ikiwemo ya kielimu.

Mkuu  huyo  wa Wilaya  ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi  katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya VIZIWI Duniani yaliyofanyika  katika kiwanja Cha Tennis  Mjini Chake Chake, Kisiwani Pemba.

Alisema wapo baadhi ya wana jamii na wananchi kwa ujumla  wamekuwa na tabia ya kuwaficha watu hao kwa madai ya kuona aibu bila ya kutambua kuwa kufanya hivyo ni kuwadhalilisha na kuwakosesha haki za msingi ambazo wanapaswa kuzipata kama watu wengine.

Aidha alisema hafurahishwi na watu wenya tabia za kuwadhalilisha watu hao na kutoa wito kwa jamii kuacha kuwadhalilisha watu hao na badala yake kuwafanyia mazuri kama watu wengine ili wasijiskie kuwa wametwengwa katika Jamii  kutokanana na hali zao.

Alisema Serikali imekuwa akiwathamini watu hao kwa kutengeneza mazingira rafiki ambapo kwa sasa imeshajenga Shule ya Elimu Mjumuishi Kisiwani Pemba,ili kuona watu wa aina hiyo wanapata elimu iliyobora kama watu wengine  ili  waweze kujiendeleza kimaisha.

‘’Wapo baadhi ya  watu wemkuwa wakiwaficha watu wenye ulemavu kwa kuwafungia ndani  jambo hilo linawadhalilisha, watu wanapaswa kutokuwaficha na wanapaswa kuwatoa ili  waweze kupata haki zao za msingi kama watu wengine’’alisema Mjaja.

Kwa upande wake Mratibu wa Baraza la Taifa la Watu wenye ulemavu Kisiwani Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, alisema kufanyika kwa maadhimisho hayo  yanajenga uwelewa kwa jamii katika kuwathamini na kupambana katika kupatikana kwa haki za watu hao.

Akisoma risala katika maadhimisho hayo Katibu wa  Chama cha Viziwi Zanzibar(CHAVIZA) Abdalla Alawi Abdalla, alisema watu wewnye ulemavu wamekuwa wakikabiliwa na Changamoto kadhaa hasa wakati wanapokwenda kutafuta huduma katika taasisi za umma kutokuwepo kwa mazingira rafiki.

Alisema Changamoto nyengine ni kukosekana kwa wataalamu wa lugha za alama kwa baadhi ya taasisi na kuishauri Serikali kuweka watalamu ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa urahisi.

Hata hivyo ameiomba Serikali kuendelea Kuboresha miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu kwenye Ofisi za Umma sambamba na kupatiwa mikopo na fursa za ajira ili kujiendeleza kimaisha.

Naye Naibu Katibu  wa Jumuiya ya watu wenye Ulemavu wa Ualbino Pemba,  Mudathir  Sharif Khatib ameiyomba Serikali kuchukua hatua kali za Kisheria kwa wale wenye tabia za kuwadhalilisha watu wenye ulemavu .

Siku ya Viziwi duniani huadhimishwa  kila mwaka  ifika Septemba 30 kwa upande wa Zanzibar madhimisho hayo yalifanyika kisiwani Pemba,huku kaulimbiyu ya mwaka huu ni dunia ambayo Viziwi popote walipo wanatumia lugha ya alama".



Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO