Hatari wanazozipata wajawazito wanaojifungulia nyumbani

                       NA FATMA HAMAD, PEMBA

MIMBA yangu ya nne manusura niiage dunia.

Katika maisha zipo siku ambazo mtu huwa  hawezi kuzisahau, iwe kwa jambo la kufurahisha au kusikitisha.

Kwa mama mmoja wa Micheweni ambaye amejaaliwa kupata watoto wanne, hawezi kuyasahau yaliyomkuta wakati akiwa na mimba yake ya pili.

Mwana mama huyu alinielezea kwa majonzi jinsi uamuzi wa kudharau ushauri wa kupata huduma za kliniki mapema na kujifungua kwa msaada wa wataalamu wa afya kulipohatarisha maisha yake.

Mama huyu aliyetaka jina lake libaki siri kati yake na mimi aliniambia…. Abadan hatasahu siku aliyopata uchungu wa uzazi na kujikuta bila ya kufahamu akiwa hospitali amewekewa chupa ya maji.

Alisema alijifungua mimba yake ya pili na  kutokwa na damu nyingi hadi kupoteza fahamu.

Baada ya kujifungua hakupata fahamu mpaka alipozinduka na kukuta amewekewa chupa ya maji katika hospitali ya Micheweni, Kaskazini Pembaa.

Mume wa huyo mama alisema baada ya kuona hali ya mke wake ni mbaya alifanya haraka kukodi gari usiku na kumharakisha hospitali.

 ndipo usiku huo alipokodi gari na kumpeleka Hospitali. Hali hi ilimpelekeakutuimia pesa nyingi ili kunusuru maisha ya mkewe na mtoto na kuiweka familia katika hali ya furaha.

‘’Nilipata funzo kubwa na muhimu. Siku hizi nikiona mke wangu anazo dalili za uchungu wa uzazi huwa namuharakisha hospitali kwa sabu huko ndiko unapopatikana ufumbuzi uhakika wa matatizo na dawa zinazohitajaika kumtibu’’, alieleza mme wake.
 

Miongoni mwa wanawake waliokutana na mitihani ya aiani hii ni Bibi Halima Juma wa Mjini Kiuyu, wilaya ya Wete, ambaye  alipata misukosuko kutokana na kulea mimba zake tatu  na kujifungulia nyumbani.

Alidai kuwa miongoni mwa mambo yaliyompeleka kutokwenda hospitali ni lugha za madaktari, nenda rudi isiyozaa matunda na hata suala la uhaba wa watalamu halimshawishi kujifungulia hospitali. .

Maryam Said mkaazi wa Chake chake ambae anaishi na virusi vya ukimwi kwa muda wa miaka 18  alimuambukiza mtoto wake wa mwanzo mambukizi ya virusi vya ukimwi.

Kwani mimba yake ya kwanza, alijifungulia nyumbani, kwa hofu ya kwenda Hospital kwa kuogopa kunyanyapaliwa.

‘’Hadi leo najilaumu, na najutia nafsiyangu, kwa kitendo cha kutokimbilia hospitali kwa ajili ya kwenda kujifungua nikidhani kwamba nyumbani ni salama,’’anasimulia.

 Kwasasa  ameshajifungua watoto  wengine watatu, ambao wako salama na vvu, baada ya kusikiliza na kutekeleza kwa vitendo ushauri wa watalamu wa afya.

Khadija Khamis mama wa watoto watano,mkaazi wa  Sizini hadi leo hii bado hajafikiwa na elimu ya kuhudhuria kliniki na ndio maana hufika kwa watalamu baina ya miezi sita hadi saba ya ujauzito wake.

 ‘’Mimi sipendi kwenda kituo cha afya ikiwa bado mimba ni changa, si pendi ile kila siku nenda na keshokutwa uje tena naona tabu,’’anfafanua.

 MTAALAMU WA AFYA HUDUMA YA MAMA NA MTOTO

Akieleza athari anazozipata mama mjazito anapojifungulia nyumbani Maryam Ali Said Mratibu wa huduma za mama na mtoto Pemba anasema moja  ni kukosekana kwa  huduma za mapema za kimataibabu kwa mama mjamzito.

 ‘’Inawezekana ikawa mama hawezi kujifungua kwa njia ya kawaida, analazimika afanyiwe upereshini, lakini mkunga wa jadi hana taluma ya kujua hilo,’’anaeleza.

  Anasisitiza kuwa kuhudhuria kituo cha afya kuanzia wiki ya mwanzo ya ujauzito hadi kufikia kujifungua ni lazima kwa mjamzito ili kujikinga na majanga.

‘’Kujifungulia nyumbani ni sawa na kununua mauti, ya mama na mtoto wake, maana hakuna mtalamu, vifa vya kinga ya maradhi na wengine wanaishi mbali na vituo vikuu vya afya,’’anasema.

Fatma Suleiman Daudi msimamizi wa huduma ya mama na mtoto katika Hospital ya Chake chake, anaeleza kuwa     mjamzito akijifungulia nyumbani, anaweza kumuambukiza maradhi mtoto wake na  mkunga.

‘’Kama mama atakua ana mambukizi kama vile  Homa ya Ini au Virusi vya ukimwi bila ya kutumia kifaa chochote, anaweza kusababisha mtoto, mkunga kupata mambukizi,’’ anaeleza.

 Mjamzito anaejifungulia nyumbani, anaweza kupata athari kiwemo kukaa kwa muda mrefu na uchungu, jambo ambalo linaweza likapelekea kuchanika haraka kwa fuko lake la uzazi.

‘’Mara nyingi wanapokuja Hospitali inakua mama ameshachoka, hali taabani, mpaka iwe wameshashindwa, hata ukija ukitoa tena izo tiba muda umeshapita,’’ afafanua mtaalamu.

Alifahamisha kuwa unapochanika kwa fuko la uzazi maranyingi mama hutokwa na damu nyingi ambayo inaweza kusababisha hata kifo chake.

‘’Unapochanika kwa fuko la uzazi, hatuwezi kusema kama ndo mwisho, lakini kama hukuwahiwa mapema kupatiwa matibau unaweza ukapoteza maisha,’’anafafanua.

 ‘’Kuna siku tulimpokea  mama na alikuwa ni ujauzito wake wa tatu, alivyo kuja akapelekwa kwenye chumba cha kujifungulia, kabla ya kumlaza kwa ajili ya kujifungua, tulimuhisi kalala kumbe ameshafariki,’’anasimulia.

Amina Omar Msellem mkaazi wa Chake chake anasema amejifungua mimba saba na zote ni kituo cha afya, wala hajapata changamoto yoyote yeye wala  watoto wake.

Abdala Nassor  Abdala mwananchi wa Chake chake anasema mama anapojifungulia nyumbani, mazingira  ya usafi Pamoja na usalama wa mama kujifungua salama yanakua hayatoshelezi.

Mkewake amejifungua mimba nane na zote alikua anampeleka Hospitali wakati anapoumwa tu na uchungu,’’anafahamisha.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja anasema ni vyema kwa wizara ya Afya kuongeza mkakati wa  elimu ili wanawake washawishike kujifungulia hospitali.

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui anasema wizara imeimarisha miundombinu  ya kutolea huduma Hospitalini, ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

 Afisa Mdhamin wizara ya Afya Khamis Bilal Ali amewataka wahudumu wa afya kuwa na lugha nzuri kwa wajawazito ili iwe ni sehemu ya ushawishi ya kuhudhuria kliniki.

‘’Wizara kwa upande wake inaendelea kuimarisha miundombinu bora ikiwemo vifaa tiba dawa, lakini ni nafasi kwa watalamu wetu wa Afya nao kutumia lugha laini ili kufanikisha hilo’’,anasema.

 TAKWIMU

Kwa mujibu wa takwimu kutoka ofisi ya mama na mtoto Pemba,inaonyesha kuwa  kwa mwaka 2022 mama 2019 walijifungulia nyumbani, kati ya hao  wane [4] walifariki.

Waliojifungulia Hospital ni 16269 kati ya hao, Micheweni ni 985, Mkoani 754, Wete 9445 na Chake chake 5365, ambapo waliofariki kutoakana na uzazi ni 15.

 Takwimu zinaonyesha kuwa kuanzia  Januari hadi Juni mwaka huu, wajawazito waliojifungulia nyumbani ni 1450, kwa upande wa wilaya ya Mkoani walikua ni  270, Chake chake 99, Micheweni 230 na Wete ni 292.

Ingawa wanaojifungulia Hospital kwa Pemba ni 8481, ambapo kwa  wilaya ya Mkoani ni 1562, Chake chake 2601, Wete 2140 na Micheweni 2178, huku vifo vikiwa tisa [9], ambapo Wete na Micheweni kulikuwa na vifo vitatu vitatu.

SERA NA SHERIA.

Sera ya wizara ya Afya ya Zanzibar ya mwaka 1990 ni kuhakikisha inaimarisha huduma za afya ya uzazi ya mama na mtoto, ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na vya watoto wachanga.



Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO