KUKIMBIA KWA WATUHUMIWA KUNACHANGIA KUONGEZEKA KWA UDHALILISHAJI
NA FATMA HAMAD, PEMBA
UKIMBIAJI wa watuhumiwa wa matukio ya
udhalilishaji ni moja ya sababu inayokwamisha kesi za udhalilishaji zisiendelee
na kushindwa kupata hatia.
Wakizungumza
katika mkutano wa kuwasilisha ripoti za udhalilishaji za mwaka 2023,huko ofisi
za Tamwa Chake chake, wanamtandao wa kupambana na udhalilishaji kisiwani Pemba
wamesema jambo ambalo limeonekana ndio muaraubaini wa kumaliza kesi za
udhalilishaji, ni kuwakimbiza watuhumiwa wa makosa hayo.
‘’Kesi
zinakaa kwa muda merefu vituo vya Polisi ukiuliza unambiwa inafanyiwa
uchunguzi, lakini ukiangalia huyo mtuhumiwa mwenyewe alishakimbia, sasa sjui
anafanyiwa uchunguzi nani, kweli hivi tutafika wapi jamani,’’walisema.
Walieleza
kuwa kuna mchezo maalumu umekuwa ukichezwa kwa makusudi wa kuwatorosha
watuhumiwa,ili kesi zisiendelee katika vyombo vya kutolea haki.
Mapema
mwanamtandao kutoka wilaya Wete Rashid Hassan Mshamata alisema kila mmoja kwa
nafasi yake kuwa na umakini wa hali ya juu, kuepuka makosa madogo madogo,
kuanzia vituo vya mkono kwa mkono hadi mahakamani, ili kukwepa mianya ya
kutorosha na kuachiliwa huru kwa watuhumiwa.
‘’Kuna siku daktari alikosea kuandika tarehe
tu, ya ile aliyo mhudumia muhanga, hapo wakili alipata njia na alin’gan’gania
hapo hapo,’’alieleza Shamata.
Kwa upande
wake mwanamtandao kutoka wilaya ya Mkoani Haji Shoka alieleza kuwa ili kuona kesi
hizo zinamalizika na kupatikana kwa hatia ni vyema kila mmoja kwa nafasi yake
kuwacha rushwa muhali.
‘’Unaweza ukampeleka muhanga Hospitali
ukambiwa ni mzima hajafanyiwa lolote,lakini ukimuangalia hata kukaa kitako
hawezi, tunakwenda wapi, turudini kwa mwezi Mungu janai,’’ alieleza Haji Shoka.
Nae Afisa
msimamizi wa mradi wa Tumia jukwaa la habari kumaliza vitendo vya udhalilishaji
Zaina Abdala Salim aliwapongeza wanamtandao hao kwa juhudi waliozichukua dhidi
ya mapambano hayo, huku akiwataka kuendelza juhudi zao hizo, ili kuona
udhalilishaji imekua historia Zanzibar.
Kwa mwaka
2023 Jumla ya kesi 27 zimeripotiwa katika wila ya Mkoani, ambapo 18 zipo
Polisi,1 imepata hukumu na fine, 1 fine, 3 zimeondolewa mahakamani kwa kukosa
ushahidi, 4 zinaendelea Mahakam.
kwa upande
wa wilaya ya Micheweni kuliripotiwa jumla ya kesi 21, ikiwa kesi 3 zilimalizika
kwa kutolewa fain pamoja na fidia kwa sababu ilikua ni za watoto,7 zipo
upelelezi na watuhumiwa tayari walishakimbia,4 zinaendelea mahakamani, 1
inasubiri kipimo cha DNA, 2 zilifungwa kwa amri ya Dpp, 1 iliachiwa huru
kutokana na kukosa ushahidi, na 1 inasubiri tathmini ya ustawi.
Na Wilaya ya
Wete kuliripotiwa kesi 45, ambapo 25 zipo upelelezi, 5 zipo DPP, 9 zinaendelea Mahakamani, 2 zilipata hukumu,na 2 zilifutwa
kwa kukosa ushahidi.


Comments
Post a Comment