KITUO CHA AFYA CHA TAJWA NI CHANZO CHA WAJAWAZITO KUJIFUNGULIA MAJUMBANI
NA FATMA HAMAD,
Wananchi wanaoishi
kijiji cha Mjini Kuyu Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba, wavunja ukimya na kutoa kilio chao kutokana baada ya kuwekeza nguvu na pesa zao kwa ajili ya kujenga kituo cha afya, lakini
kimeshindwa kutumika na kutoa huduma kwa sababu ya kukosekana kwa wahudumu wa
Afya .
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao
Mwananchi khamis Omar
alieleza kuwa walifanya mchango nyumba hadi nyumba wa vifaa vya ujenzi pamoja na kushiriki
katika ujenzi na kujenga kituo cha afya, na
Serikali ikawasaidia katika
kuwezeka kituo hicho.
Hata hivyo, tokea
mwaka 2011 mpaka sasa kituo hicho hakitumiki
na kimekuwa gofu.
‘’Kituo hicho tulikijenga
kwa nguvu zetu na pesa zetu, na Serikali ikaja ikatusaidia kuezeka, ila tunashangaa Serikali
yenyewe imekitelekeza, kipotu
kinaporomoka, hakitumiki,’’alifahamisha
Khamis.
Alisema huu ni mwaka wa 12 tokea kujengwa kwa kituo hicho,
ambapo kilifunguliwa na mbio za mwenge kwa shangwe na nderemo, ili
kuondosha shida za wananchi wa kijiji hicho.
Alisema baada ya kuona
wanapata tabu kwa kufuata huduma za afya masafa marefu, ndipo wakamua wao
wenyewe kujitolea kujenga ili waondokana
na kadhya hiyo, lakini bado wanaendelea
tu kuteseka.
‘’Tunaiomba Serikali itujali na ituonee huruma, ituwekee kituo wananchi wake tunateketea,’’ alieleza
mwananchi.
Mapema mwanachi Raya Hassan
Alisema kukosekana kwa kituo cha afya karibu na makaazi yao wanapata
shida hususan wanapopata mgonjwa wakati wa usiku.
Alisema wanachukua
masafa kilo mita nne kufuata
huduma ya afya, ambapo wanalazimika
kupita sehemu za vichaka na mabonde.
‘’Hospitali ipo mbali,
na hatuna daktari kijiji kizima hichi, hivyo tunapopata mgonjwa au mzazi wa ghafla hususan nyakati za usiku inashindikana kupata
huduma kwa haraka, sisi hatujui
tumfanye nini,’’ alisema bi Raya.
Bikame Bakar
Darusi alisema kuwa kukosekana kwa kituo cha afya kunachangia
kwa kiasi kikubwa wa mama wajawazito kujifungulia
majumbani.
‘’ Mimi binafsi mtoto
wangu alitaka kujifungulia njiani, kwani
barabara yenyewe hatuna, usafiri ni boda
boda tu, gari za abiria hazifiki hususan kipindi cha mvua, hivyo wazazi wengi
huishia kujifungulia njiani,’’ aliseleza kwa masikitiko Bikame.
‘’Tunaiomba Serikali ituonee huruma tunapata shida hususan
sisi wazazi, tunaomba hichi kituo mutuekee kitoe huduma japo za zarura, japo
huduma za mama na mtoto tu,’’ alisema Bi Kame.
Alisema kuwa uzazi wa sikuhizi ni mashaka, hivyo ni vyema
kituo kiweze kutoa huduma ili kulinda usalama wa mama na mtoto.
Diwani wa wadi hiyo Bi Nasra alisema yeye pamoja na sheha tayari wameshafuatilia kila sehemu ili kuona kituo hicho kinatoa huduma, lakini imeshindikana.
‘’Ijapokuwa kinajengwa
kituo katika eneo la kiuyu minungwini, lakini ni vvyema kuwangaliwe tena kwa
jicho la pili, kwa vile kijiji cha mjini kiuyu ni kijiji cha ndani, na hakuna hata miundombinu ya barabara,’’ alieleza diwani.
Afisa mdhamini wizara ya Jinsia na maendeleo ya jamii Khamis Bilal Ali alifahamisha kuwa wanajenga Hospitali katika eneo la kiuyu minungwini ambayo
itawanufaisha wananchi wa Minungwini pamoja na wa mjini kuyu.
Alisema kuwa jingo
hilo walilolijenga watalitumia kukiwa na kesi maalumu kama vile mripuko wa
maradhi pamoja na kipindi cha utoaji wa chanjo za watoto.



Comments
Post a Comment