VIJANA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIMAENDELEO.
ZAID ya Shilingi
milioni miamoja zimetengwa na taasisi ya
SOS Zanzi bar kwa ajili ya kuwawezesha vijana ambao ni wajasiriamali ili
waweze kujikwamua kimaisha na kutimiza ndoto zao kupitia biashara ndogo ndogo.
Meneja miradi
wa Shirika la SOS Kisiwani Pemba Abdalla Omar, amesema taasisi hiyo imetenga kiasi
hicho cha fedha ili kuwasadia vijana katika nyanja tofauti ikiwemo Uvuvi. Biashara
na Kilimo hasa katika kuelekeza nguvu katika uchumi wa Bluu.
‘’Tunataka
kuwawezesha vijana ili weweze kujiajiri wenyewe jambo ambalo litawaepusha
kujiingiza katika vikundi viovu’’ alisema meneja Abdala.
Aidha
alieleza kuwa fedha hizo zitawasaidia
vijana kufanya miradi mbali mbali ya kimaendeleo ambayo itawapatia kipato kitakachowasaidia
katika familia zao.
Hivyo meneja
huyo amewataka vijana kuchangamkia fursa hizo
za kimaendeleo ili waweze kuondokana na
umaskini uliokithiri.
BaadhiyawadaukatikaKikaohichowalishauriserikalikufuatiliailimiradiyakuwawezeshavijanapamojanakuwapatiataalumasahihiyauendeshajinausimamiziwamiradi.
Comments
Post a Comment