MAKOSA 25 WIZI WA KARAFUU YARIPOTIWA POLISI KUSINI PEMBA MSIMU HUU.
Jumla
ya matukio 25 ya wizi wa karafuu yameripotiwa katika Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba tokea kuanza kwa
msimu wa mavuno ya karafuu mwaka huu.
Akizungumza
na wandishi wa habari huko ofisini kwake kamanda wa Polisi Mkoa huo Richad Tadei Mchovu amesema matukio hayo
yalioripotiwa ni wizi wa karafuu mbichi.
Aidha
amesema katika matukio hayo pia wamefanikiwa kuwashikilia vijana 27
wanaojihusisha na uhalifu wa karafuu.
Aidha
amesema katika matukio hayo makosa 12
tayari yamepelekwa Mahakamani ambapo kijana
mmoja ameshafungwa jela.
Sambamba
na hayo amewataka wananchi Kisiwani Pemba kuendelea na uchumaji wa zao la
karafuu kwa Amani bila kufanyiana
vitendo vyovyote vya kihalifu.
Amewataka
wananchi kuuza karafuu zao katika
Shirika la ZSTC, ili wawezekuisadia Serikali mapato.
Comments
Post a Comment