Rushwa muhali bado ni tatizo kukomesha vitendo vya Udhalilishaji.
Licha ya
juhudi mbali mbali zinazochukuliwa na Serikali pamoja na Asasi za kiraia
kuielimisha Jamii madhara ya Udhalilishaji wa kijinsia kwa Watoto na jinsi ya kutoa ushahidi kwa kesi hizo lakini
bado inaonekana matendo hayo yanaendelea
kujitokeza kutokana na Muhali uliopo kwa
Wanajamii.
Hayo
yamesema na wajumbe wa Mtandao wa kupinga Udhalilishaji kutoka Wilaya ya
Mkoani katika kikao cha uwasilishaji wa ripoti za utekelezaji wa
majukumu yao ya kutoa Elimu juu ya
madhara ya Udhalilishaji wa Kijinsia kwa Jamii huko ukumbi wa Chama cha
Wandishi wa habari Wanawake Tanzania Zanzibar
[ Tamwma] Mkanjuni Chake chake
Pemba. Wanajamii hao.
Wamesema Jamii
inaonekana kuyafumbia macho na kuyafanyia suluhu Mitaani matendo ya
udhalilishaji jambo ambalo linasababisha kuongezeka sikuhadi siku.
Aidha
wameeleza kuwa kuwepo kwa umasikini uliokithiri
imedaiwa kuwa ni moja ya sababu inayopelekea kuongezeka kwa udhalilishaji kwa Watoto
Comments
Post a Comment