Posts

Showing posts from December, 2024

Jamii yatahadharishwa kuachwa nyuma wanawake wenye ulemavu mradi mabadiliko tabia nchi

Image
                                   Na Fatma Hamad- Pemba …...hana mguu, hana mkono, haoni, atawezaje kutunza mazingira……. HAYO NI MANENO ya ALi   Juma Mbarouk   kiongozi wa kamati ya uhifadhi mazingira Chwale anasema wanawake wenye ulemavu ni vigumu kuingizwa kwenye kamati za utunzaji mazingira. Anasema kamati yake, ina wajumbe 15, kati ya hao hamna hata mjumbe mmoja mwanamke mwenye ulemavu. Anasema hajamshirikisha   mwanamke yeyote mwenye ulemavu, kwani anadhani hawezi kufanya shughuli hizo za uhifadhi kutokana na hali zao. ‘’Mtu aliekua hana mguu, hana mkono, wala haoni atawezaje kupambana na mabadiliko ya tabianchi hasa kwa kuwemo ndani ya kamati,’’anasema. VIONGOZI/WAJUMBE WA KAMATI Fatma Shaaban Mohamed ni kiongozi wa kamati ya kilimo mseto Shehia ya Mjini kiuyu, anasema katika kamati yake anao wajumbe 25 mtu mwenye ulemavu hana hata mmoja. Anasema hajawahi kum...

Huuhapa mkakati wa vyama vya siasa, kuwandaa wanawake kuelekea uchaguzi wa 2025.

Image
                                     Na Fatma Hamad – Pemba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililotolewa azimio   Octoba 31 mwaka 2000 limesema kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi inazidisha demokrasia ya nchi, uchumi, amani na utulivu. Eneo jengine ni katiba ya Zanzibar ya 1984 katika kifungu cha 21 (1) kinaeleza   kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu mwanamke   na taifa lake. Hata Sera ya Chama cha Mapinduzi   kwenye mkakati wake, ni kuongoza umma wa watanzania katika ujenzi wa uchumi wa kisiasa,   utakaoleta   maisha bora ya wananchi kwa kuwawezesha   kiuchumi.   Kwa mujibu wa   Mkataba wa Kikanda wa Nchi za Kusini mwa Afrika,   uliotiwa saini mwaka 2008 kupitia kifungu nambari 13 cha mkataba huo,   kinaelezea   kuwekwa   mik...

Wanawake wawagaragaza wanaume, katika kamati za uhifadhi mazingira za shehia

Image
                          Na Fatma Hamad- Pemba Rais Samia Suluh Hassan wa Tanzania, mara baada ya kula kiapo Machi 19, 2021, alitaja moja ya vipaumbele vyake, ni kuyashirikisha makundi mbali mbali wakiwemo wanawake. Na ndio maana wapo mawaziri kadhaa wanawake wanaoongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwemo waziri wa Afya Jenister Mhagama, na mwenzake   Ashatu Kijaji anashikilia wizara ya Mifugo na uvuvi. Lakini hata wizara ya Fedha na mipango, inashikiliwa na mwanadada   Natu Elmaamry Mwamba kwa nafasi ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo. Eneo jingine ni uwepo wa sera ya taifa ya Jinsia na maendeleo ya mwaka 2023/2033 ambayo nayo imehimiza, uzingatiaji wa haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake na wanaume. Kwa Zanzibar katiba ya mwaka 1984, kifungu cha 10 (e) kimeleza kila raia atakuwa na haki sawa, majukumu na fursa sawa kwa mujibu wa sheria.   Ndani ya bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jins...

Jeshi la Polisi lawataka wahisani kuisaidia familia ya wototo wenye ulemavu

Image
                                NA FATMA HAMAD – PEMBA Jeshi la  Polisi  Mkoa wa Kusini Pemba limewataka  Wadau  pamoja na wahisani mbali mbali  kujitokeza kuisaidia  familia ya Mohamed Mussa yenye watoto  wawili wenye ulemavu wa viungo, iliyopo  Matele wilaya ya Mkoani Pemba mahitaji muhimu ikiwemo  makaazi pamoja na viti mwendo. Wito  huo umetolewa na Mratibu  wa  Polisi  jamii wa mkoa wa Kusini Pemba Makame Nasibu Silima kwa niaba ya Kamanda wa Polisi  wa  Mkoa huo,  Abdla Hussein Mussa,  mara  baada ya kukabidhi msaaada wa vyakula na godoro,  ikiwa ni shamra shamra ya kuelekea madhimisho ya siku  16  za  kupinga  ukatili  wa kijinsia. Alisema mazingira ya familia hiyo ni duni, hivyo ni vyema wadau pamoja na wahisani kujitokeza kuisaidia familia hiyo ili iweze kuishi katika hali ya furah...

WAANDISHI WA HABARI MSHICHOKE KUDAI MABADILIKO YA SHERIA.

Image
  Na Fatma Hamad- Pemba Waandishi wa habari wamehimizwa kuendelea kuzipigia kelele Sheria za habari ziweze kurekebishwa, jambo litalopelekea kuondosha khofu na woga kwa wanahabari hao. Akizungumza katika mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo juu ya kufanya ushawishi na utetezi kwa Sheria za habari, kwa wandishi wa vyombo mbalimbali vya habari, Afisa programu kutoka Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar Zaina Abdala Mzee, amesema ipo haja kwa wandishi wa habari kupaza sauti zao kwa kuzisemea Sheria hizo, ili kuona kilio chao kimepatiwa ufumbuzi. Afisa huyo ameyasema hao huko ukumbi wa Tamwa Chake chake Pemba, ambapo amesema endapo kilio cha wandishi wa habari kitazingatiwa na kupatikana kwa Sheria mpya za habari,  kutasaidia wandishi wa habari kufanya majukumu yao bila ya khofu wala woga wowote. ‘’Kama kutapatikana Sheria mpya ambayo itakua haina vifungu vinavyokwaza uhuru wa habari, kutawasaidia wandishi kufanya kazi zao wakiwahuru,’’ameeleza. Akita...

Mkakati wa Polisi kwa wagombea wanawake katika Uchaguzi wa 2025

Image
  NA FATMA HAMAD-PEMBA Ni wakati sasa wa dunia kutambua umuhimu wa wanawake katika uongozi,  kwani wanapokua  katika  ngazi za maamuzi  ni chachu ya kuondosha ubaguzi wa kijinsia, na kuleta maendeleo  ya  kiuchumi,  kijamii  na  kisiasa. Hata hivyo idadi ya ushiriki wa wanawake katika vyombo vya maamuzi bado ni mdogo, hivyo ipo haja kuwekwa mikakati madhubuti, ikiwemo kutekeleza sheria ambazo zinazingatia mazingira salama naya uwazi kwa wanawake kuweza kushiriki katika uongozi. Na ndio maana  Serikali ya mapinduzi Zanziba ikafanya marekebisho  ya sheria ya  vyama vya siasa Zanzibar  ya mwaka 2024,  ili kuondosha baadhi ya vifungu ambavyo vimekua ni kandamizi kwa wagombea wanawake. Kutokana  na  hayo  wenzetu   wa Jeshi  la  Polisi Zanzibar  likaja na mkakati  makhsusi kwa ajili ya kuwalinda wagombea wanawake dhidi ya vitendo vya udhalilishaji,  ili kuona wanakua s...