Posts

Showing posts from June, 2024

WANAOJISHUGHULISHA NA BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA CHA MOTO KUKIONA

Image
                                       Na Is-haka Moh`d-Pemba Waziri waNchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Harusi Said Suleiman amewaomba Wazazi/Walezi Visiwani Zanzibar kufuatilia kwa karibu nyenendo za watoto wao ili kuwalinda kutumbukia katika   janga la utumiaji wa dawa za kulevya. Waziri Harusi ametoa ombi hilo wakatia kifungua kongamano la siku ya maadhimisho ya siku ya kupiga vita matumizi na usafirishaji wa dawa za kulevya duniani ambapo kwahapa   Zanzibar Kitaifa yameanzimishwa leo Juni 27 katika ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi Chake Chake Pemba. Alisema utumiaji wa dawa za kulevya umekuwa ukiathiri kwa kiasi kikubwa kwa vijana walio na umri kati ya miaka 9 na 45 ambapo vijana wengi huanza kutumia matumizi ya dawa za kulevya wakiwa katika Skuli za ...

WANDISHI WA HABARI WAPEWA MBINU

Image
                                                NA FATMA HAMAD,PEMBA Wandishi wa habari wametakiwa kujikita zaidi Vijijini, kuibua na kuziandika kero zinazowakwaza Wananchi ili ziweze kufahamika na kupatiwa ufumbuzi. Wito huo umetolewa na Katibu wa Mwavuli wa Asasi za Kiraia kisiwani Pemba (PACSO) Sifuni Ali Haji katika mkutano uliowakutanisha wandishi wa Habari pamoja Asasi za kiraia huko ukumbi wa Maktaba kuu Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema wananchi hususan wa Vijijini wamekuwa wakikumbana na matatizo kadhaa ikiwemo Maji, Bara bara na Udhalilishaji, hivyo endapo mtazisemea zinaweza zikatatuliwa kupitia malaka husika. ‘’Wandishi wa habari nyinyi ndio mdomo wa wanyonge, wasemeeni ili muweze kuwaokoa na matatizo,’’alisema.   Mapema mwenyekiti wa P...

WANAWAKE WENYE ULEMAVU WAOMBA USHIRIKISHWAJI KWENYE MICHEZO

Image
                                NA FATMA HAMAD,PEMBA Katika kuelekea siku ya mtoto wa Afrika duniani Makamo mwenyekiti wa Jumuia ya wanawake wenye ulemavu Zanziba Hidaya Mjaka Ali ameitaka jamii kuwashirikisha watoto wa kike wenye ulemavu katika harakati mbali mbali ikiwemo Michezo   ili nawao wapate fursa zilizomo katika Nchi. Akizungumza na mwandishi wa habari huko ofisini kwake Mkanjuni Chake Chake Pemba anasema watoto wa kike wenye nawao wana haki ya kushiriki michezo kama watoto wengine. Alisema jamii imekuwa akiwachukulia watoto wenye ulemavu kwamba hawawezi kushiriki michezo kutokana na ulemavu wao. ‘’Ukimuelekeza, na ukimjenga vizuri mtoto mwenye ulemavu mboana anaweza akacheza na akafanya vizuri,’’alisema. Alisema ni wakati kwa jamii kuondokana na itikadi potofu, na badala yake wawashirikishe   watoto wenye u...

UVCCM YAOMBA KUFUNGIWA KWA MTANDAO WA KIJAMII WA X

Image
                                                                              NA FATMA HAMAD,PEMBA. Umoja wa vijana  (UVCCM)  Mkoa wa Kaskazini Unguja umeiyomba  Serekali ya Jamhuri ya Muungano na ile ya Zanzibar,kuuchukulia  hatua mitandao ya kijami X (TWITTER) ikiwemo kuufungia ambao wamedai unakwenda  kinyume na madili ya vijana wa  Tanzania. Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Ismail Ali Ussi alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Mjini Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema Serikali inapaswa kuangalia kwa karibu na  kuufungia mtandao huo ...

WANANCHI WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUPATA MATIBABU

Image
                                 NA FATMA HAMAD,PEMBA Wananchi wa mkoa wa Kaskazini Pemba wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika kambi ya uchunguzi na matibabu iliyopo Micheweni uwanja wa kwa mshaame mata, ili waweze kuchunguzwa na kujulikana matatizo yao na kupatiwa tiba. Wito huo umetolewa na mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib wakati akizungumza na wananchi wa mkoa  huo katika uzinduzi wa kambi ya Uchunguzi na Matibabu iliyoandaliwa na tasisi ya Zanzibar Maisha bora Fondation huko Micheweni Pemba alisema matibabu hayo yatatolewa bure kwa wanachi wote. Alisema lengo la Serikali  ya Mapinduzi ni kuona wananchi  wanaishi wakiwa na afya njema, hivyo ni vyema kila mwenye matatizo kufika katika kambi hiyo ili aweze kuchunguzwa na kupatiwa huduma bora za afya. ‘’Taifa bora linajengwa na jamii iliyo bora, hivyo msione tabu kuja kupata tiba kwani ni bure,’’alisema Alisema enda...

USHIRIKI MDOGO WA WATOTO WA KIKE WENYE ULEMAVU WA AKILI KWENYE MICHEZO

Image
Wadau waanisha vikwazo, kimo cha mtazamo hasi, miundombinu isiyorafiki Wenyewe wadai kutengwa, kuanzia ngazi ya familia, jamii NA FATMA HAMAD, PEMBA SERIKALI, ya Mapinduzi ya Zanzibar imeandaa utaratibu mzuri wa kuwaendeleza watu wenye mahitaji maalum.   Watu wenye ulemavu wamekuwa wakishiriki katika shughuli za michezo na kwa kiasi kikubwa wameweza kujipatia heshima wao na taifa, kwa kushinda katika mashindano mbali mbali.   Licha ya juhudi za serikali katika kuhakikisha kundi hilo, linapata haki zao kama watu wengine hasa katika kushiriki katika mashindano yanayoandaliwa ndani na nje ya nchi, imekuwa tofauti kwa baadhi ya watu, kuwaficha watoto wa kike wenye ulemavu.   Kwani wanayohaki ya kushirikishwa katika nyanja zote za kiuchumi, kama raia wote, bila ya kujali ulemavu wao, maana kinachoangaliwa sio ulemavu wao, ni haki zao na uwezo wao. Haki ya kushiriki katika harakati za kimaendeleo, imeelezwa kwenye ibara ya 9 ya mkataba wa kimataifa wa watu wenye ...