WANAWAKE WATAKIWA KUSHIRIKIANA ILI WAWEZE KUJILETEA MABADILIKO
Mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mama Zainab Kombo Shaib, ametoa wito kwa wanawake nchini kushikamana ili kuweza kujikomboa kutokana na ukubwa wa wimbi la changamoto zinazowakabili
.Baada ya kikao hicho Mama zainab alipata fursa ya kukutana na watoto yatima na wenye Ulemavu wa Shehia ya Kinyasini na Mtemani za Wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba.
MKE
wa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Mama Zainab Kombo Shaib, ametoa wito
kwa mamlaka zote pamoja na asasi za kiraia, kuimarisha afya ya mama na mtoto,
ili kujenga ustawi bora wa jamii, utakaochangia maendeleo ya nchi. Mama
Zainab ameyasema hayo leo katika ziara yake, alipotembelea Hospitali ya
Vitongoji, Wilaya ya Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba. Amesema
afya ya mama na mtoto ni sehemu muhimu ya msingi wa ustawi wa jamii,
unaolenga kuzalisha na kuendeleza nguvu kazi ya Taifa, na hatimaye
kufanikisha juhudi za kujiletea maendeleo. "Afya
zikiwa vizuri hata uzalishaji unaongezeka, hivyo ni vyema kuzitumia
rasilimali tulizonazo kwa uangalifu katika kutoa huduma bora za kijamii
ambazo ni pamoja na afya ya mama na mtoto," amesema Mama Zainab. Akitoa
nasaha zake mbele ya madaktari na wahudumu wa hospitali hiyo, Mama Zainab
ameahidi kupaza sauti kwa wadau wa afya ili kusaidia kuzitatua changamoto,
zikiwemo za uhaba wa vifaa, hasa katika wodi ya akinamama wajawazito na
sehemu ya kujifungulia. Aidha
ametoa wito kwa madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo kuendelea kuchukua
tahadhari na kuwaelimisha watu juu ya athari za mripuko wa janga la CORONA. Naye
Daktari dhamana wa Hospitali ya Vitongoji, Dokta Sharif Khatib ameeleza
shukran zake za dhati kwa kufanikiwa kupata kifaa kipya cha kupimia damu na
utambuzi wa maradhi mbali mbali cha ‘HAEMATOLOGICAL ANALYZER’,
kitakachosaidia ufanisi wa huduma za hospitali hiyo kwa wananchi. Mama
Zainab ambaye ameambatana na Bi. Awena Masoud Sanani, Mke wa aliyekuwa Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad, katika
ziara yake kisiwani Pemba, ametembelea maeneo mbali mbali yakiwemo Jengo la
Bohari ya Dawa la Vitongoji, kabla ya kuelekea Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa
Kaskazini Pemba. Katika
ziara hiyo, Bi Zainab ameongoza zoezi la kuwapatia misaada mbali mbali
wagojwa na watu wasiojiweza, ikiwemo sabuni, pempasi, mipira ya kusaidia
kujifungua kwa akina mama pamoja na mashuka ya vitanda vya hospitali. Akikabidhi
vifaa hivyo Mama Zainab ametoa wito kwa wananchi kujitokeza katika kusaidia,
ijapokuwa kwa kiasi kidogo, ili kuwapatia unafuu wanyonge na kuwatatulia
changamoto zinazowakabili. Akitoa
salamu za wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Micheweni, Bi Mgeni Khatib Yahya
amesifia juhudi za utendaji mzuri zinazotekelezwa na wahudumu wa Hospitali ya
Micheweni, licha ya changamoto ya kuhudumia idadi kubwa ya wananchi kila
siku. Mkuu
huyo wa Wilaya amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano na wauguzi wa
Hospitali hiyo iliyopanda daraja hadi Hospitali ya Wilaya kuanzia Agosti 30
mwaka huu, ili pia kusaidia kufanikisha malengo ya Serikali. Naye
Afisa Mdhamini wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto
Bw. Yakoub Mohd Shoka amesema ujio wa Mama Zainab katika ziara hiyo ni faraja
kubwa, huku akitoa wito kwa viongozi wengine kufuata nyayo zake katika
kuimarisha na kuendeleza Sekta ya Afya. *Kitengo
cha Habari* *Ofisi
ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar* 04/10/2021
|
|
Comments
Post a Comment