WIZARA HABARI YATAKIWA KUINGIZA TIMU ZHA NETBAL KATIKA MASHINDANO YA MAWIZARA
SALIM HAMAD,PEMBA
MDAU wa Michezo Kisiwani Pemba Raya Mkoko Hassan ,Ameishauri
Wizara ya Habari Vijana Sanaa na Michezo ambayo inaanda michuano ya
mawizara kuingiza timu za Netbal katika mashindano ya Mawizara ili
kuona akina mama nao wanapata nafasi za kuonesha Vipaji vyao.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi alisema Wizara ya habari
inapaswa kuangalia suala hilo kwani nao akina mama wana uwezo mkubwa wa
kupambana kwenye mashindano kama hayo.
Alisema kuwepo kwa mashindano hayo kwa upande wa Netbali itakuwa
ni jambo zuri ambalo litasadia kukuza uhusiano na Afya zao kutokana na
kuwa michezo ni afya.
Alisema kafuatia mashindano hayo yamewapa hamasa wanawake nao
kuona wanakuwemo kwenye mashindano hayo kwa kila wizara kuwepo kwa timu moja ya
wanawake ili waweze kufika mbali.
Comments
Post a Comment