‘’Wandishi endeleeni kuipigia debe Sheria ya habari, ili irekebishwe’’

NA FATMA HAMAD, PEMBA

Wandishi wa habari wametakiwa kuendelea kuipigia kelele Sheria ya habari, kuona imefanyiwa marekebesho na  kuondoshwa vifungu vinavyokwaza  uhuru wa habari na vyombo vya habar.

Alisema wandishi wa habari ndio wahanga wakubwa ambao wanaathirika kutokana na kuepo  kwa Sheria inayominya uhuru wao kwani inapelekea kukosa baadhi ya tarifa.

Akizungumza na wandishi wa habari katika mkutano wa tathmini wa mradi wa  kudai uhuru wa habari, Afisa miradi na tathmini kutoka Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar Mohd Khatib Mohd, alisema kukosekana na sheria rafiki hakuathiri wandishi wa habari pekeyao bali hata jamii kiujumla.

 Hivyo Afisa huyo alisema  kuepo kwa hilo, ipohaja kuendelea kuandika habari zinazoshawishi  kufanyiwa marekebisho na kupatikana kwa Sheria mpya Zanzibar.


Mapema akiwasilisha ripoti ya mapitio a Sheria za Habari  Afisa programu kutoka Tamwa, Zanzibar Zaina Abdalla Mzee, alisema licha ya juhudi mbalimbali zinazochukuliwa kupiga kelele kupatikana kwa Sheria mpya za habari, bado halijafanyiwa kazi ipaswavyo, ingawa Baraza la Wawakilishi limeahidi kuifanyia kazi  kwa mwaka  ujao.

Alisema wamewajengea uwezo wandishi wa habari kuvifahamu vifungu vinavyokandamiza uhuru wao, waweze kuvifahamu na kuvisemea virekebishwe, na kuwekwa vingene vipya ambavyo vinaendana na muda.

Alisema jumla ya makala na vipindi 237  zimeandikwa na wandishi wa habari kwa muda wa mwaka mmoja, ambazo zimekua zikishawishi serikali kuona umuhimu wa kupatikana kwa sharia mpya ya habari Zanzibar.

"Miongoni mwa matokeo ya mradi huu ni pamoja na kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari kuzitambua Sheria za Habari kuona mapungufu yaliyomo katika Sheria hizo, kutoa mapendekezo ili ziweze kufanyiwa marekebisho" alisema 


Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO