Posts

Showing posts from February, 2025

Wasaidizi wa sheria wapewa mbinu

Image
                   NA FATMA HAMAD- PEMBA Wasaidizi wa Sheria  wametakiwa kuendelea  kutoa elimu kwa jamii juu ya masuala ya udhalilishaji, ili kuona inaondokana na vitendo  hivyo viovu ambavyo  vimekua  vikijitokeza siku  hadi  siku. Akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wasaidizi wa sheria wa wilaya ya Micheweni  Muhasibu wa Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya hiyo  Riziki Ali Hamad juu ya masuala ya udhalilishaji, huko Tumbe wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema katika wilaya ya Micheweni  bado kumekua kukijitokeza masuala ya ubakaji na ulawiti  kwa watoto, hivyo ipohaja kwa wasaidizi wa sheria kuisaidia jamii kwa kuwaelimisha madhara yatokanayo na  masuala hayo,  ili kuona yameondoka. Akitaja  sababu inayopelekea kujitokeza kwa masuala hayo ya ubakaji na ulawiti  katika wilaya hiyo ni utelekezwaji uliokithiri wa wanawake na wato...

Tunahitaji kupatiwa maji, tuzalishe mazao kwa wingi ili tujikomboe na umaskini

Image
                                             NA FATMA HAMAD –PEMBA KUKOSEKANA KWA HUDUMA za Maji safi na salama imekua ni kero kubwa kwa wakulima   wanaolima   kilimo msitu katika Shehia za Mjini kiuyu,    Kambini kichokochwe, Mchanga mdogo na Chwale wilaya ya Wete   Mkoa wa Kaskazini Pemba.   Akizungmza na mwandishi wa habari mara baada ya kuwatembelea katika mashamba yao mkulima Fatma Sheha Juma kutoka Kiuyu minungwini anasema wanahitaji kupatiwa maji katika mashamba yao, ili waweze kukuza vilimo vyao. Alisema wanapata shida kubeba maji majumbani kwao na kupeleka katika mashamba yao, hivyo wanahitaji kupatiwa msaada wa kuchimbiwa visima karibu na maeneo yao wanayolima, ili waweze kuzalisha mazao kwa wingi. ‘’Kwakweli kubeba maji kwa vichwa   kutoka majumbani hadi mashambani   kwetu tunakolima ni shida   tunaathirika, hi...

Yafahamu madhara anayopata mwanamke wakati akijiwekea vitu katika sehemu zake za siri

Image
                     NA FATMA HAMAD - PEMBA   Wanawake wametakiwa kuacha tabia ya kuweka vitu kwenye sehemu za siri, kwani wanaweza kuathiri mfumo mzima wa viungo vya uzazi.   Hayo yamesemwa na Mratibu wa Tume ya Ukimwi Pemba (ZAC) Ali Mbarouk Omar   wakati Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania (TAMWA) ZANZIBAR Ofisi   Pemba, alisema, wapo baadhi ya wanawake huweka vitu katika sehemu zao za siri, jambo ambalo ni hatari kwa afya ya uzazi.   Alisema kuwa, ni vyema wakaenda   hospitalini na vituo vya afya kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa mara kwa mara, endapo wamepata matatizo waweze ili waweze   kupatiwa matibabu na sio kuweka vitu ambavyo vinaweza kuwapatia madhara zaidi.   "Kuna baadhi yao huweka vitu kama wanajitibu baada ya kupata magonjwa ya kujamiiana na kuna wengine wanaweka vitu hivyo kwa urembo, haya yote hayafai kwa...

Aliniambia Ami Hakimu anaekaa kwa da Fatma ndie aliemfanya.

Image
                            NA FATMA HAMAD-PEMBA SHAHIDI NAMBA TANO ZUWENA HASSAN Mohamed ambae ni jirani   alieleza Mahkama ya Mkoa Chakechake kwamba, muathirika alimuambia kuwa aliemfanyia  kitendo hicho ambacho kilimpelekea kulazwa Hospitali,  ni ami Hakimu ambae anakaa  kwa da fatma.   Shahidi huyo alidai kuwa  Julai 15 mwaka jana aliondoka nyumani kwake yeye na mtoto wake na  kwenda Hospitali ya Abdala Mzee  Mkoani kwa ajili ya matibabu yake ya Figo. Alidai kuwa  baada ya kufika Mkoani mtoto wake alimuaga na kumwambia anakwenda msalani (chooni ) kujisaidia, nayeye  akabakia na kusubiri andike cheti kwa ajili ya kwenda kwa Daktari. Aliporudi msalani yulele mtoto wake alimuambia kuwa alimkuta babayake  akiwa amekuja na mtoto wa shangazi yake Hospitali. ‘’Aliponiambia  babayake yuko na mtoto wa shangazi yake anamatatizo, nilipandisha  ha...

Jitihada za vyama vya sisa wanazozifanya kwa wanaume, juu ya uongozi kwa mwanamke

Image
                     Na Salim Hamad-Pemba Suala   la   uongozi     ni   haki   ya    raia    wote   na sio kwa       wanaumme   pekeo . Kwani Haki ya uongozi imetajwa   katika Kifungu cha 21 (3)   cha Katiba ya Zanzibar     ya   mwaka 1984   kinasema   kila   Mzanzibari   anayohaki   ya kushika   nafasi   yoyote   ya   kazi   na   shughuli   yoyote   iliyoko   chini   ya Mamlaka   ya   Zanzibar. Sera na Sheria mbalimbali za Zanzibar zimeelekeza kutambua haki ya mwanamke kushiriki katika demokrasia na uongozi. Historia   inatuonesha kwamba uislamu unaruhusu mwanamke kuwa kiongozi, kwani wapo wanawake kadhaa ambao walishiriki   nafasi za mamuzi   wakati wa Mtume Muhammad (S.A. W). Ambapo miongoni   mwa wanawake waliosh...