Wakulima waikumbusha jambo Serikali
NA FATMA HAMAD, PEMBA Wananchi kisiwani Pemba ambao walikatiwa mikarafuu yao kwa ajili ya kupisha miundombinu ya umeme wameiomba Serikali ya Mapinduzi kuwalipa fidia zao wakulima hao. Wakizungumza katika hafla ya ugawaji wa zawadi kwa washindi wa Vuna na Tigo pesa mkulima Khamis Juma Khamis na Halima Mohamed Seif huko Makonyo Chake chake Pemba walisema walikatiwa mikarafuu yao na kuahidiwa kulipya ila hadi leo hakuna chochote walichokipata. Walisema kuwa karafuu ndio zao kuu wanalolitegemea kujipatia kipato, hivyo ni vyema Serikali kulikalia kitako na kuhakikisha wanalipatia ufumbuzi suala hilo. ‘’Tulikatiwa Mikarafuu yetu na tukaahidiwa tutalipwa ila hadi sasa hakuna lolote tulilolipata’’,walisema. Mapema mkulima Ali Kombo Hamad alisema katika msimu wa karafuu ujao ni vyema shirika la biashara la ZSTC kuboresha miundombinu ya kiwanda cha kununulia Makonyo kilichopo wawi, kuhakikisha kinafanya kazi ili kuwaondoshea usumbufu wananchi wanao kuja kuuza makonyo yao. ‘’Tulichuku...