WANDISHI WA HABARI WAONESHWA NJIA

 
  NA FATMA HAMAD,PEMBA

Wandishi wa habari wametakiwa kujikita zaidi Vijijini  kuibua kero zinazo wakwaza Wananchi  ili ziweze   kupatiwa ufumbuzi.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud katika hafla ya madhimisho ya Uhuru wa vyombo vya habari Duniani huko Gombani Kisiwani  Pemba.

Amesema wananchi wamekua wakikabiliwa na kero mbali mbali katika vijiji vyao, hivyo kama waandishi watawezakuziandikia zitaweza kutatua kwa haraka.

‘’Ndugu zangu wandishi wa habari  msishie tu kuandika habari za Mkuu wa mkoa kasema, Mkuu wa wilaya kasema, nendeni vijijini mkaibue shida  za Wananchi ili tupate kuzisikia na tuweze kuchukua hatua za kuzitatua’’alisema Mattar.

Aidha Mattar alisema uwandishi wa Habari  unanafasi kubwa katika jamii kwa  kuwafikiwa wasiokuwa na sauti  hivyo amewataka waandishi hao kuelekeza nguvu zao katika kuandika Habari za Vijijini.

‘’Fani ya Uwandishi wa Habari  ni sauti ya wasiokuwa na sauti shukeni Shukeni kwa wananchi kutafuta changamoto za Wananchi tupate kuzifahamu’’alisema Mattar.

 Kwa upande wake Afisa mdhamini wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mfamau Lali Mfamau aliwasisitiza wandishi wa habari kufuata Miko na Madili ya kazi yao ili waweze kuandika habari zenye ukweli ambazo zitaleta tija kwa Jamii na Taifa kwa ujumla.

Aidha  mdhamini huyo alisema anasikitishwa na baadhi ya Viongozi wa Serikali kuwatumia watu ambao sio wandishi wa habari kufanya shughuli za kihabari, hali ambayo inakwenda kinyume na Sheria. 


 

 
Nae mwenyekiti wa Jumuia ya wandishi wa habari kisiwani Pemba (PPC)Bakar Mussa Juma alisema kuwepo kwa uhuru wa habari kunachangia wandishi wa habari kuandika habari ambazo zitaleta mabadiliko  kwenye jamii.
 
 


 


 

Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’