Posts

Showing posts from May, 2024

WANDISHI WA HABARI WAPEWA SOMO

Image
                                                NA FATMA HAMAD,PEMBA Wandishi wa habari wametakiwa kuandika habari ambazo zitaihamasisha Jamii kulipa kipaumbele suala la michezo kwa wanawake ili kuona nawao wanashiriki katika mashindano mbali mbali Nchini. Wito huo umetolewa na Mkufunzi wa mafunzo ya masuala mbali mbali ya Jinsia na michezo Hawra Shamte wakati akizungumza na wandishi wa habari huko Ukumbi wa   Tamwa Chake chak Pemba. Alisema bado Jamii hawampi kipaombele mwanamke kushiriki katika masuala ya michezo kutokana na dhana iliyojengeka kwamba mwanamke anaeingia kwenye michezo ni muhuni. ‘’Tumegundua kwamba Michezo yote ya wanawake imekufa kutokana na mfumo dume ambao umetawala katika Jamii ya Wazanzibar kwani wanasema michezo kwa mtoto wa kike ni uhun...

MAMA AJIFUNGUA NA KUMFUKIA MTOTO MCHANGA

Image
    PICHA NA MAKTABA                      NA FATMA HAMAD, PEMBA   Mama mmoja anayefahamika kwa jina la Mchanga Omar Said anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 35 mkaazi wa Kijiji cha Sizini Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba,anadaiwa   kumfukia mtoto mchanga mara   baada ya kujifungua.    Mama huyo akiwa kwa sasa ni mjane akiwa na watoto saba ambaye alitengana na Mwenza wake kwa zaidi ya miaka miwili ambapo kwa sasa anashiliwa na Jeshi la Polisi.  Akizungumza juu ya tukio hiilo Mkuu wa Wilaya ya Micheweni, Mgeni Khatib Yahya, alisema Jumamosi Mei 18 saa 5 asubuhi alipokea   taarifa za mama huyo kuwa alijifungua   na alichojifungua hakikuonekana,   Wananchi walifuatilia suala hilo na kugundua kuwa mama huyo alijifungua na kisha kumfukia mtoto kibandani mwake.   Mkuu huyo wa wilaya alisema alimwita mama huyo na kuzu...

WANDISHI WA HABARI WAONESHWA NJIA

Image
      NA FATMA HAMAD,PEMBA Wandishi wa habari wametakiwa kujikita zaidi Vijijini   kuibua kero zinazo wakwaza Wananchi   ili ziweze    kupatiwa ufumbuzi. Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud katika hafla ya madhimisho ya Uhuru wa vyombo vya habari Duniani huko Gombani Kisiwani   Pemba. Amesema wananchi wamekua wakikabiliwa na kero mbali mbali katika vijiji vyao, hivyo kama waandishi watawezakuziandikia zitaweza kutatua kwa haraka. ‘’Ndugu zangu wandishi wa habari   msishie tu kuandika habari za Mkuu wa mkoa kasema, Mkuu wa wilaya kasema, nendeni vijijini mkaibue shida   za Wananchi ili tupate kuzisikia na tuweze kuchukua hatua za kuzitatua’’alisema Mattar. Aidha Mattar alisema uwandishi wa Habari   unanafasi kubwa katika jamii kwa   kuwafikiwa wasiokuwa na sauti   hivyo amewataka waandishi hao kuelekeza nguvu zao katika kuandika Habari za Vijijini. ‘’Fani ya Uwandishi wa Haba...

KUKOSEKANA KWA MTANDAO KWA SABABISHA HASARA KWA WAFANYA BIASHARA

Image
  NA NIHIFADHI ABDULLAH UNGUJA  Kukosekana kwa mtandao kumesababisha hasara ya kutoingiza kipato kwa watu ambao shughuli zao zinategemea huduma hiyo kwa kiasi kikubwa  Wakizungumza na kati fm kwa nyakati tofauti wafanyakazi wanaotoa huduma ya intanet na waandishi wa habari wa mitandao wamesema hali hiyo imewarejesha nyuma kwani walishindwa kufanya kazi.  Waandishi wa habari Hassan Mselem  na Amina Masoud wamesema kutokana na dunia ilipo kuzimwa au kukosekana huduma ya inteneti  inapelekea hasara sio tu kwao bali hata kwa wananchi kutopata habari kwa wakati muafaka  Nae Juma Marijani amesema ameamua kujiajiri kwa kuekeza kutoa huduma za intanet hivyo inapokesakana kunarejesha nyuma nguvu za kujikwamua kiuchumi  Sambamba na hayo ametoa wito kwa serikali kutatua vikwazo katika masuala ya mtandao ili kwenda sambamba na ulimwengu ulipo  

WANAHABARI, WADAU WAOMBA VIFUNGU VINAVYOMINYA UHURU WA HABARI VIREKEBISHWE

Image
                                                NA FATMA HAMAD,PEMBA KILA baada ya miaka 10 sheria huwa zinahitaji kubadilishwa ili kuondosha mapungufu ya vifungu ambavyo vitakua haviendani na utekelezaji wa sheria hiyo.   Ijapo kuwa wakati mwengine sio lazima kusubiriwe hadi itimie miaka 10 ndio   iweze kufanyiwa marekebisho. Na hii itasaidia kuweka sawa vifungu vyenye mapungufu ili viweze kuendana na muda na mazingira ya sasa. Lakini tukiangalia sheria ya Usajili wa Uwakala wa habari, Magazeti na Vitabu namba 5 ya mwaka 1988 iliyofanywa marekebisho na Sheria Namba 8 ya mwaka 1997, haiendani na mazingira ya sasa kwani ni  kongwe hivyo inahitajika ifanyiwe marekebisho. Takriban ni miaka 26 tangu Sheria hiyo kufanyiwa marekebisho ingawa bado baa...