Posts

Showing posts from April, 2025

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO

Image
                       NA FATMA HAMAD – PEMBA SHAHIDI  BASHE  MAKAME  Khamis  ambae  ni Afisa kutoka Maabara ya Mkemia mkuu wa Serikali  Zanzibar ameiambia Mahkama ya Mkoa iliyopo Wete  Kaskazi Pemba, k baada ya kufanya uchunguzi wa vinasaba katika Mashine ya DNA vipimo vimengudua kwamba mtuhumiwa Bahati  Mashauri ndie baba mzazi wa mtoto aliezaliwa na binti aliembaka. Akitoa ushahidi wake  mbele ya Mahkama hiyo ya Mkoa  Bashe alidai kuwa baada ya kupokea vinasaba vya mtoto aliezaliwa na vya mtuhumiwa  pamoja na mama aliezaa baada ya kubakwa, alianza kufanya uchunguzi wa  vinasaba  vya mtoto na mtuhumiwa  na kugudua kwamba mtuhumiwa  ndie baba  mzazi wa mtoto kwa asilimia 9.99 Aidha alidai kuwa  aliendelea  kufanya vipimo  vya  vinasaba vya mtoto na mama yake  pia aligundua kwamba  mtoto ndie mama yake mzazi binti ambae...

WAKULIMA BADO WALIA NA BEI NDOGO YA MWANI

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA WANAKIKUNDI CHA TUMAINI kilichopo shehia ya Michenzani Mkoani Pemba ambacho kinajishughulisha na ukulima wa  kilimo  cha Mwani,  wametupa kilio chao kwa  Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar  kuwangalia  tena   kwa jicho  la  huruma, kwa  kuongeza  bei  ya  mwani. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi  mwanakikundi Biwanu Ngwali Faki  alisema bei ya mwani ya kilo shilingi miasaba (700)  ni ndogo, ukilinganisha na gharama wanazozitoa wakati wa kulima. Alisema lengo la Serikali ya Mapinduzi ya awamu ya Nane ni kuwaimarisha wakulima wa Mwani kichumi, hivyo ni wakati kuongeza bei hadi shilingi 2000.   ‘’Kwaweli bei ya shilingi miasaba inatuumiza kazi ni ngumu, ukiangalia Tunanunua Kamba pamoja na taitai kwa gharama kubwa,hivyo tunaiomba Serikali ituengezee bei, ifike angalau elfu 2000,’’ alisema. Kwa upande wake mwanakikundi Kazija Ali Bakar  alisema  bado wakulima wa ...

WADAU WALIA NA SHERIA ZINAZOKWAZA HAKI YA KUPATA HABARI

Image
                         NA FATMA HAMAD - PEMBA Baada ya kilio cha muda mrefu waandishi wa habari visiwani Zanzibar   wana matumaini makubwa juu ya kupata sheria mpya za habari ambazo hazina vikwazo kwao na zinazoendana na mazingira ya sasa. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika hotuba zake kadhaa amekua akizungumzia changamoto ambazo zimekua zikiikabili tasnia ya habari na kuahidi kuzitatua changamoto hizo, ili kuona vyombo vya habari vinatekeleza majukumu yake vikiwa huru. ‘’Tunatambua changamoto zinazovikabili vyombo vya habari pamoja na waandishi wa habari, hivyo Serikali itafanya kila jitihada kuviwezesha, ili kuona wandishi wa habari wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi,’’alisema Rais Mwinyi Dokta Mwinyi katika miaka minne ya uongozi wake amekua ni kiongozi   wa   mwanzo na wa mfano katika nchi hii kukutana mara kwa mara na waandishi wa habari Visiwani Zanzibar, am...

SHERIA ZA HABARI ZANZIBAR BADO KIZUNGUMKUTI

Image
  NA FATMA HAMAD - PEMBA Katika sheria ya usajili wa uwakala wa habari, magazeti na vitabu namba 5 ya mwaka 1988 iliyofanyiwa marekebisho na sheria no 8 ya mwaka 1997 yapo maneno kadhaa yaliyotumika ambayo yanaonekana kuwa na mapungufu na ambayo yanakwaza uhuru wa vyombo vya habari. Matumizi   hayo ya maneno yaliyotumika katika sheria hiyo yanaweza kuathiri   uhuru wa habari pamoja na waandishi wa habari ikiwa hayatofanyiwa marekebisho. Katika makala hii   tutaangalia   sheria   ya usajili wa uwakala wa habari, magazeti na vitabu namba 5 ya mwaka 1988   iliyofanyiwa marekebisho na sheria no 8 ya mwaka 1997 ina muda wa   miaka 36 sasa,   ambapo katika vifungu vyake inayo maneno ambayo sio rafiki kwa vyombo vya habari na waandishi wa habari. Miongoni mwa maneno hayo yenye kuleta ukakasi yanapatikana katika kifungu cha 30 cha Sheria   ya usajili wa uwakala wa habari, magazeti na vitabu namba 5 ya mwaka 1988 kama ilivyofanyiwa marek...