Posts

Showing posts from November, 2024

Jumuiya za vyama vya siasa, muarubaini wa kuwasaidia wanawake kwenye uongozi

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA MWENYEKITI wa CUF   Mhamed Haji Kombo, wa Chake chake akiri kuwa uanzishwaji wa jumuia za wanawake ndani ya vyama vya siasa, zimesaidia kwani zimewaamsha wanaume kufahamu kwamba, haki ya kugombea ni kwa wanachama wote. Aanasema jumuia za wanawake zimezaa matunda kwani wanawake katika Chama chao wamekua na uthubutu wa kugombea nafasi za ungozi, ambapo ngazi za kitaifa viongozi wengi ni   wanawake. ’ ‘Wamekuwa wakipata elimu na mafunzo mbali mbali   kwenye jumuia zao, na ndo maana wakawa na uthubutu huo wa kuhodhi nafasi za uongozi,’’ Amesema Mohamed wakati wa mahojiano. Mwenyekiti wa Chama cha ACT WAZALENDO Mkoa wa Kusini Pemba kichama, Saleh Nassor Juma anasema mchango wa Ngome za Wanawake ni mkubwa kwani zimewafanya wanawake waondokanae na hofu ya kugombea na kushika nyadhifa za uongozi.   ‘’Kwa kweli hizi Jumuia za wanawake kwenye vyaama zimewatoa hofu wanawake, maana ukiangalia kwenye kamati yetu ya   uongozi ya Mkoa Cha...

Wananchi wa Njuguni wampa tano sheha wao

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA WANANCHI wa shehia ya Wingwi Njuguni Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wamesema, kuwepo kwa sheha mwanamke katika shehia yao kumewasaidia kupata mambo mbali mbali ya kimaendeleo, ikiwemo huduma za maji safi na salama.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini kwao Njuguni wamesema, kupata sheha mwanamke katika shehia yao wameimarika kiuchumi na kimaendeleo, kwani wamepata huduma ambazo ilikua ni kilio cha muda mrefu. Wamesema wakati wa uongozi wa sheha aliepita, vijiji vingi vilikua havina huduma ya maji safi kama vile Pwana, Mtemani, lakini ndani ya mwaka mmoja baada ya kukaa sheha mwanamke, vijiji vingi ambavyo vilikua havina maji vimefikishwa huduma hiyo. ‘’Kwa kweli sheha wetu huyu tunajivunia sana, maana amekuwa mtetezi wa hali ya juu ya mambo mbali mbali ambayo yamekuwa yakitukwaza,’’wameeleza. Aidha, wamesema kwamba pia katika shehia yao kumeanzishwa timu malumu ya mpira wa miguu, ikiwa na lengo la kuinua vipaji vya vijana kat...

Gharama za Chaguzi bado kikwazo kwa wanawake wanaotaka kugombea

Image
  NA FATMA HAMAD,PEMBA Wanawake Kisiwani Pemba ambao wanania ya kugombea wameitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar pamoja naya Mungano kuhakikisha wanapunguza vikwazo ikiwemo gharama  za uchaguzi, ili kuona nawao wanaingia kwa wingi majimboni na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi. Wakizungumza kwa nyakati tofauti baaadhi ya wanawake ambao waligombea Uchaguzi uliopita wa 2020,walisema ili kuona wanawake wanajitokeza kwa wingi kuchukua fomu za uongozi ni vyema kupunguza vikwazo ambavyo vinawafanya washindwe kugombea. Tumu Mwalimu mkaazi wa Wingwi ambae aligombea Ubunge jimbo la Wingwi  kupitia Chama cha Mapinduzi CCM alisema bado suala la uchukuaji wa fomu za kugombea ni gharama kubwa, hali inayopelekea wanawake wasio na uwezo kushindwa kujitokeza majimboni, jambo linalopelekea wenye pesa zao kuyahodhi majimbo. Amesema Kwa mujibu wa utaratibu ulivyo, anaetaka kugombea uwakilishi anatakiwa alipie chamani shilingi laki 100,000 kwa kuchukua fomu. Pia ameeleza kua anatakiwa kul...

Masheha watakiwa kuwashirikisha wanawake kwenye kamati zao

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA Sheha wa Sizini Suleiman Shaame Hamad, amewataka masheha wenzake kuhakikisha wanazingatia suala la usawa wa kijinsia katika Kamati zao, ili kuona wanawake nawao wanapata fursa kupitia kamati hizo. Sheha huyo ametoa wito huo wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwake Sizini, amesema ni wakati sasa kwa masheha kuhakikisha wanatekeleza dhana ya Jinsia kwa kuwashirikisha wanawake katika Kamati zao, kwani kutawapa fursa ya kujiamini, na kua viongozi wazuri wa badae. Amesema unapompa nafasi yoyote mwanamke ni rahisi,  kufanikiwa, kwani wao ni wachapakazi na ni washauri wazuri hasa katika nyanja za maendeleo. ‘’Binafsi nimeona nilipowashirikisha wanawake katika kamati yangu, maendeleo yamepatikana, ukilinganisha na hapo nyuma,’’amesema . Amesema miongoni mwa faida ambazo amezipata baada ya kuwashirikisha wanawake katika Kamati yake, amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi, kwani ameanzisha shughuli za u...