VIJANA WATAKIWA KUJIWEKEZA ZAID KWENYE MICHEZO

 

NA FATMA HAMAD, PEMBA

Vijana wamehimizwa  kujikita  zaidi katika suala la  michezo hasa mpira wa miguu ambao umekuwa na mchango mkubwa wa ajira.

Hayo yamesemwa na Mkaguzi wa Ulinzi shirikishi kutoka shehia ya Pandani na  Mlindo Khalfan  Ali Ussi mara baada ya kumalizika kwa  Fainali ya mpira wa miguu kati ya kikundi cha ulinzi shirikishi cha kijiji cha Masipa na Miburani, huko uwanja wa Pandani wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema mpira ni moja ya sehemu ya  kujipatia ajira, hivyo wakati umefika kwa vijana kujiunga na mpira wa miguu, jambo ambalo litawawezesha kujipatia fursa zilizomo kwenye michezo.

‘’Mpira sasahivi umekuwa ni biashara kubwa Duniani, hivyo acheni kukaa tu kwenye vigenge kwa kisingizio kwamba hamna kazi ya kufanya, alisema.

Alieleza endapo Vijana watajishughulisha na michezo wataepukana na matendo maovu ikiwemo Ubakaji,Ujambazi na Wizi.

Alisema lengo la  mashindano  hayo ni kuwa weka pamoja na kuwashajihisha vijanahao kujiunga pamoja na kupanga mikakati zaidi ya kupambana na changamoto zilizomo katika Shehia zao.


Nao Vijana hao  walimuahidi mkaguzi  huyo  kwamba  wataendelea  kuwasimamia  na kuwapa Elimu  wale  ambao hawajakuwatayari  kuacha  vitendo  vya  kihalifu ili kuhakikisha  wanaishi kwa Amani  Vijijini mwao.

 Kwa upande wao  badhi ya wazazi waliohudhuria  mchezo huo walimpongeza  mkaguzi huyo, huku wakimtaka aendelee kuwa karibu na Vijana hao na kuwapa elimu juu ya kujitambua, ili wasijingize katika makundi maovu, na kuona wanakuwa watoto wenye madili mema.

Katika mtanange huo Masipa ilibuka na ushindi Penalti Nne kwa Tatu zidi ya Miburani.

 

 

 

 

 

  .

 

 

 

 

 


 

 

 




 


 

 

 

 

 

  .

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.