JAMII YAHIMIZWA KUITUNZA AMANI



NA FATMA  HAMAD PEMBA.

 Wadau waliopatiwa  mafunzo ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya mani wamehimizwa  kuendelea kuielimisha jamii kujiepusha  na migogoro isiyo ya lazima ambayo itapelekea uvujifu wa amani Nchini.

Akizungumza na wadau waliopatiwa mafunzo ya utatuzi wa migogoro  kutoka Tasisi mbali mbali Kisiwani Pemba Afisa ufuatiliaji na tathmini kutoka kituo cha huduma za Sheria Zanzibar Khamis Haroun Hamad amesema  badojamii imekabiliwa na migogoro mbali mbali hivyo ipo haja kuendelea kutolewa kwa elimu ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani ili kuona wanasuluhishana wenyewe kwa wenyewe bila ya kuekeana visasi.

‘’Migogoro ya Ardhi pamoja na ndoa imeonekana kwamba ndio inayoshamiri katika jamii hivyo ipo haja kwa wadau hao kuchukua jitihada za makusudi kuielimisha jamii kuchukuwa hatua stahiki  pindi  unapotokezea mgogoro  jambo ambalo litasaidia kuepusha  mivutano  na mifarakano kwao’’ alisema Afisa ufuatiliaji.

Aidha amesema bila ya kuepo kwa amani hakuna maendeleo yoyote hivyo amewasa  wanajamii kuifanyia kazi elimu hiyo  wanayopewa na kuepuka viashiria  ambavo vinaweza vikasababisha kutoweka kwa amani iliyopo.

Nao wadau hao wameiomba Serikali ya mapinduzi Zanzibar kupunguza gharama za upatikanaji wa hatimiliki ili kila mtu aweze kumudu kuinunua jambo ambalo litaepusha kutokea  kwa migogoro  kwa jamii.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.