WANDISHI WATAKIWA KUWA WALIMU WAZURI KWA JAMII JUU YA UTUNZAJI WA AMANI

Wandishi wa habari wametakiwa kuwa mstari wa mbele kuielimisha Jamii kujiepusha na migogoro  amboyo inaweza kupelekea uvunjifu wa Amani.

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa jumuia ya Wandishi wa habari Kisiwani Pemba [PPC] Bakar Mussa Juma wakati akifungua mafunzo ya siku mbili  juu ya utekwelezaji wa mradi wa Sauti yangu, Amani yangu ndio khatma yangu kwa wandhishi wa habari huko Gombani Chake chake.

Amesema wandishi wa habari wanamchango mkubwa wa kuisaidia  jamii, hivyo ni budi kutumia taaluma yao kwa kuielimisha juu ya  athari zinazojitokeza wakati kunapokua na migogo.

‘’ Nyinyi wandishi mnaaminika katika jamii, hivyo ipeni elimu jamii ili isiwe katika migogoro na badalayake ibaki salama’’ Alisema mwenyekiti PPC.

Aidha amesema bila ya kuepo kwa Amani hakuna lolote linaloendelea, hivyo ni vyema watu wanapokoseana kuvumiliana na kusuluhishana jambo ambalo litapelekea kuwepo kwa maendeleo na kudumu kwa Amani Nchi iliyopo sasa.



Kwa upande wake mwenyekiti mstaafu wajumuia ya wandishi wa habari [PPC] Said Mohd Ali amewaasa wandishi wa habari kuepuka kuandika habari za uchochezi ambazo zinaweza zikaleta mfarakano na mivutano katika Jamii.

‘’Wandhi andikeni habari zenye ukweli na zenye faida kwa jamii, msiwe chanzo cha migogoro’’Alisema mwenyekiti mstaafu.



Ali Masoud Kombo mwandishi kutoka redio jamii micheweni ambae ni miongoni mwa waliohudhuria mafunzo hayo amewataka wandishi wenzake wajiamini na wasiwe  na woga wakati wanapokua katika majukumu yao ilimradi tu wafuate Miko, Kanuni na Madili ya kazi yao.

Mradi wa Sauti yangu, Amani yangu ndio khatma yangu unaotekelezwa  kwa muda wa miezi sita na Jumuia ya wandishi wa habari Pemba [PPC] kwa kushirikiana na shirika la Seach for Comman Ground Foundation  chini ya ufadhili wa umoja wa Nchi za  ulaya.[European Union



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.