RUSHWA BADO NI TATIZO KWA WAGOMBEA WANAWAKE KISIWANI PEMBA.
Akizungumza kwa masikitiko Hadia Omari Dadi katika
mkutano wa uhamasishaji wa mwanamke kugombea nafasi za uongozi, huko Wingwi
wilaya ya Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba alisema unapofikia wakati wa uchaguzi suala la rushwa
hujitokeza kwa wingi katika vyama jambo ambalo linawakosesha wanawake wenye
kipato duni kushindwa kujinyakulia nafasi mbalimbalizauongozimajimboni.
Alisema
inaonekana wengi wanaopata nafasi hizo ni wale wenye nacho,auwaleambaotayariwalishakaakwenyeuongozikwakipinchama.
‘’Mimi
mwenyewe binafsi nishagombea mara tatu ila kwa sababu ni masikini, sina pesa
nimeshindwakupatanafasiyoyoteilekutokanasinauwezo,’’Alisemabia.
Alifahamisha
kuwa Rushwa ni adui mkubwa anekwamisha maendeleo, hivyo tunaishauri Serikali
ya Mapinduzi kujipanga upya katika mwaka 2025 kupambana na viongozi wa
vyama vya siasa ili kuona uhalifu huo umeondoka na kuona wanyonge nawao
wanapata nafasi.
Sambamba na
hilo aliitaka pegao kutoa elimu kwa
Viongozi wa vyama vya siasa kutoa fursa kwa wale ambao wanasifa za uongozi
nasio kumchagua mtu kwa sababu tu ana pesa zake, hali ambayo inarudisha nyuma
maendeleo ya wananchi.
Akichangia katika mkutano huo Khamis Mohd Nassor pia alisema kuwa ni kweli wanawake wengi wa vijijini wanaishi katika mazingira magumu, lakini bado ile elimu hasa ya kujiingiza katika uongozi haijawaingia ipasavyo, jambo ambalo linawafanya wanaume kujichukulia fursa mbali mbali za kimaendeleo.
Nae mmoja wa
wahamasishaji wa mwanamke kugombea
nafasi za uongozi Khalfan Amour Mohd alisema lengo la mkutano huo ni
kuwafahamisha Wanawake kufahamu kuwa uongozi ni suala la mwanamke na mwanamme,
na sio tu kama jamii inavyodai mwanamke hafai kuwa kiongozi.
Comments
Post a Comment