kijana huyu mwenye ulemavu wa viungo ashindwa kwenda skuli kwa kukosa kibaskeli cha maringi mawili

Licha ya juhudi zinazochukuliwa na Serikali pamoja na Asasi mbali ili kuona  watu wenye ulemavu na wao wanapata haki  zao stahiki, lakini bado watu hao wanaendelea kukumbana na changamoto kadhaa na kupelekea kudumaa kwa maendeleo yao.

Hayo yamebainika kwa  Kijana Anifu Jeilani Issa  mwenye ulemavu wa Viungo  (14) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tano Skuli ya Msingi Ole Wilaya ya Chake Chake Pemba, kushindwa kuhudhuria Skuli kwa kukosa Kibaskeli cha magurudumu mawili.

Akizungumza kwa masikitiko  Mama Mzazi wa Mtoto huyo huko Nyumbani kwake Ole Mihogoni   amsema ni Zaidi ya miezi minne hivi sasa mototo wake Anifu hajahudhuria Skuli kuungana na wenzake kusoma kufuatia changamoto hiyo. 

‘’ alikua nacho kigari lakini sasahivi kimeharibika, jambo ambalo linapelekea kukosa masomo yake’’ Alisema mama mzazi 

Hivyo mama huyo amewaomba wahisani pamoja na wasamaria wema kupatiwa msaada wa kigari ili kuweza kushiriki kikamilifu katika masomo yake kwa vile hivi sasa anashindwa kuhudhuria kwa  kukosa kibaskeli cha magurudumu mawili. 

‘’Naomba msaada nipatiwe kibaskeli mtoto wangu aendeleze masomo yake ili aweze kutimiza ndoto zake.


Aidha Mama huyo amesema mototo wake Anifu  anapenda kusoma shule na madrasa kutokana na ufahamu mzuri alionao kijana  huyo.

Nae Mratibu wa Kitengo Cha Elimu Mjumuisho kutoka Wizara ya Elumu na Mafunzo ya Amali  Kisiwani Pemba,Halima Mohd Khamis amesema Kitengo hicho kimekuwa kikichukua juhudi mbali mbali katika kuwasaidia watu wa aina hiyo lakini bado wanashindwa kulimaliza tatizo hilo kutokana na uhitaji wa Vifaa hivyo kwa watu wenye mahitaji maalumu.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.