WANDISHI WATAKIWA KURIPOTI MATATIZO YAO MCT WAKATI YANAPOWATOKEZEA


 

WAANDISHI wa habari nchini, wametakiwa kushirikiana na Baraza la Habari Tanzania [MCT] kutoa malalamiko yao wakati wanapopata matatizo katika majukumu yao ya kazi.

Hayo yamesemwa na Afisa ufuatiliaji na tathmini wa MCT  Paul Mallimbo  wakati akizungumza na wandishi wa habari huko Zanzibar, ambapo amesema Baraza kwa kuwajali wandishi wa habari, limeweka utaratibu wa kupokea kero zinazowakumba ikiwemo kupigwa, kutukanwa, kunyimwa taarifa ili kuweza kutoa msaada kwao.

Amesema imeonekana bado wandishi hawajakuwa na mwamko wa kuripoti matatizo yao, wakati yanapowatokezea na jambo ambalo linawanyima fursa yao ya kufanya kazi zao kwa umakini.

Kwa upande mwengine ameitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kutoa mashirikiano ya hali ya juu wandishi wa habari, jambo ambalo itawafanya waweze kuandika na kuripoti habari zenye ukweli na zenye kuleta mabadiliko mazuri katika Jamii.

Mapema Mtendaji wa Baraza la habari Tanzania [ MCT] ofisi ya Zanzibar Shifaa Said Hassan, amewasihi wandishi wa habari kushirikiana kwa pamoja katika majukumu yao ya kazi, jambo ambalo litawawezesha kufanya kazi zao kwa uwadilifu wa hali ya juu.



Nao baadhi ya wandishi waliohudhuria mkutano huo wamesema, wapo baadhi ya wandishi wanakumbana na vikwazo tofauti katika kazi zao, lakini bado wanakaa kimya jambo ambalo linawafanya waendelee kunyanyasika siku hadi siku.





                     

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.