WANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUWAPA ELIMU JAMII JUU YA USULUHISHAJI WA MIGOGORO


 

Wandishi wa habari wametakiwa kuwaelimisha jamii kwa kuandika habari za utatuzi wa migogoro kama ya Siasa, Ndoa ili waweze kujiepusha na migogoro isiyo ya lazima.

Akizungumza katika mkutano juu ya namna ya utatuzi wa migogoro katika Jamii Afisa ufuatiliaji na tathmini kutoka kituo cha huduma za sheria Zanzibar Khamis Haroun Hamad huko gombani Chake chake Pemba.

Amesema  wandishi wana nafasi kubwa katika jamii hivyo ni wajibu kutumia kalamu zao kwa kuielimisha jamii kujiepusha na migogoro isiyo ya lazima jambo ambalo litapelekea kuvunjika kwa Amani.

Amesema suala la kulinda amani si la mtu peke yake bali kila mmoja kwa nafasi yake anapaswa achukue tahadhari juu ya kulinda haki za mwenzake.



Mapema mratibu wa mradi wa Jenga amani yetu  kutoka kituo cha huduma za sheria Zanzibar Jamila Masoud amesema wakati umefika kwa wandishi wa habari kujikita zaid Vijijini katika kazi zao jambo ambalo litawasaidia kuibua migogoro ambayo inajitokeza na kuweza kuzitolea suluhu.



Nao baadhi ya washiriki wa mkutano huo wamesema imeonekana migogoro ya Ardhi pamoja na kindoa ndio inayojitokeza zaid katika Jamiim, hivyo  ipo haja kuwepo na mashiriano ya pamoja kati ya wadau na viongozi wa mradi huu kuelekeza nguvu zao zaid katika maeneo hayo  ili kuona jamii inaondokana na hilo.




Mafunzo hayo yaliojumuisha wadau mbali mbali wakiwemo wandishi wa habar, mahakama ya Ardhi, Dawati la jinsia, Masheha ambapo  lengo la mradi huo ni kuona jamii inadumisha amani  yameandaliwa na shirika la Seach fer Common Ground kwa kushirikiana na Kituo cha huduma za Sheria Zanzibar, Kituo cha sheria na haki za binadamu kwa ufadhil wa Umoja wa ulaya.






Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.