WANDISHI WA HABARI WAHAMASISHENI WANAUME KUPIMA VVU





Wandishi wa hababari wametakiwa kuandika habari za Afya ya jamii ambazo zitatoa hamasa kwa Wanaume ili waweze kujitokeza Hospitali kupima VVU.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa tume ya ukimwi Zanzibar  [ZAC] Ahmed Mohd wakati akizungumza na wandishi wa habari huko Gombani chake, amesema wandishi wana mchango mkubwa juu ya kuwaelimisha wanaume kupima afya zao jambo ambalo litaepusha ongezeko la mambukizi mapya ya virusi vya ukimwi Nchini.

Amesema imebainika kuwa idadi ya wanaume wanaojitokeza  vituoni mwa afya kupima VVU ni ndogo ukilinganisha na wanawake.

‘’Wanaume bado hawataki kupima afya zao, wengi ni wanawake ndio wanaozitumia huduma hizo,’’Amesema dk Ahmed.

Amesema  wanaume wengi wanaogopa kupima  vvu kutokana  na kutokuwepo kwa usiri kwa baadhi ya madaktari wanaotoa huduma hizo, jambo ambalo linachangia  kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa mambukizi mapya ya virusi vya ukimwi.

Amesema wanaume wengi kipimo chao kikubwa ni wake zao, kwani wanahisi wakishakwenda kupima na kuonekana wako salama na wao  hujihisi hawana mambukizi.

Ameeleza kuwa tokea kugundulika ugnjwa huo hapa  Visiwani mnamo mwaka 1986 wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wameweza kudhibiti mambukizi hadi kufikia 0.4

Akitaja idadi ya watu wanaoishi na vvu hapa Zanzibar ni 7020 ambapo wanawake ni 4828, wanaume ni 2,192, wanaotumia dawa kwa upande wa wanawake 4774 na wanaume ni 2168.



Mapema kaimu mratibu wa  tume ya ukimwi ofisi ya Pemba Ali mbarouk Omar amesema wandishi  wa habari wana nafasi kubwa katika kuwashajiisha wanaume kushiriki katika huduma za afya.



Nae mkufunzi wa mafunzo hayo Abuu bakar Ibrahim Msemo amesema wakati umefika kwa wandishi wa habari kuandika zenye kuonyesha tabia hatarishi ili wanaume waweze kuzifahamu na kujiepusha nazo.




Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.